Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday, 2 March 2017

MTOTO WA MAREHEMU JOHN KOMBA ATOA WIMBO KUUNGA MKONO MAPAMBANO DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA


Na Bashir Nkoromo
IKIWA sasa ni takriban miaka miwili tangu aliyekuwa Mkurugenzi wa Tanzania One Theatre (TOT), Kampteni John Komba, kufariki Dunia, Mtoto wake Gerald John Komba, ameibuka na kutoa wimbo wa kuiunga mkono Serikali katika mapambano yake mapya dhidi ya dawa za kulenya nchini Tanzania.

Gerald aliyezaliwa mwaka 1986 jijini Dar es salaam, amesema, ameamua kutoa wimbo huo wenye maudhi ya kwaya, ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya kifo cha Baba yake, Marehemu John Komba aliyefariki  Dunia, Februari 28, 2015 katika Hospitali ya TMJ, Mikocheni jijini Dar e Salaam, alikopelekwa baada ya kuzidiwa ghafla akiwa nyumbani kwake, Tangibovu kwa Komba.

Mtoto huyo wa Jihn Komba aliyekuwa mwanamuziki nguri wa utunzi na uimbaji wa nyimbo za kwaya, amesema, wimbo aliotoa nimarejeo ya wimbo ambao ulitungwa na nguri huyo, kukemea usambazaji na matumizi ya dawa za kulevya miaka zaidi ya kumi iliyopita, lakini baada ya kuurekodi haukuwahi kuimbwa na TOT wala kuchezwa kwenye vituo vya Radio au Televisheni.

Gerald ambaye amesomea Sheria katika Chuo Kikuu cha Saint Augustine kilichopo Mwanza,  Tanzania,  baada ya masomo ya shule ya Msingi katika shule ya Kawe "A" na shule yasekondari Mbezi Beach High school, anasema katika kuutoa wimbo huo, hakubabaisha kwa kuwa na yeye anacho kipaji cha kuimba japo amekuwa hakitumii sana.  BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.


RAIS MAGUFULI AANZA ZIARA YA SIKU NNE MIKOA YA PWANI,LINDI NA MTWARA



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania Dkt.  John Pombe Magufuli, leo  Machi 02, 2017 ameanza ziara ya kikazi ya siku 4 katika Mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.

Katika ziara hiyo Rais Magufuli atafungua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara.

Leo asubuhi Rais Magufuli ataweka jiwe la msingi la kiwanda cha kutengeneza vigae (Tiles) cha Tanzania Goodwill Ceramic Tiles Ltd. kilichopo Mkuranga Mkoani Pwani na baadaye ataelekea Mkoani Lindi.

Kesho Machi 03, 2017 Rais Magufuli ataendelea na ziara yake Mkoani Lindi na keshokutwa  Machi 04, 2017 atafanya ziara yake Mkoani Mtwara.


Wednesday, 1 March 2017

HABARI YA HIVI PUNDE: RAIS MAGUFULI AMTEUA MAMA SALMA KIKWETE KUWA MBUNGE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 01 Machi, 2017 amemteua Mhe. Salma Kikwete kuwa Mbunge  wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Salma Kikwete ni Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mhe. Salma Kikwete ataapishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zitakazotangazwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


TAZAMA VIDEO YA RAIS MAGUFULI NA RAIS MSTAAFU MKAPA WALIPOSALI JUMATANO YA MAJIVU DAR ES SALAAM LEO.


OFISI YA MAKAMU WA RAIS YAHAMIA RASMI DODOMA

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora akipokewa na watumishi wa Ofisi yake Mjini Dodoma na kusalimiana na Isaya Kisiri Afisa Ugavi Mwandamizi mara baada ya kuwasili katika Ofisi zilizopo `Area D` Dodoma.Kulia ni Oigenia Mpanduji Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora akipokewa na watumishi wa Ofisi yake Mjini Dodoma mara baada ya kuwasili katika Ofisi zilizopo `Area D` Dodoma na kusalimana na Oigenia Mpanduji Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Eng. Ngosi Mwihava (kushoto) akiongea na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais mjini Dodoma.


TAASISI YA MOYO YA JKCI KUPELEKA WATOTO NANE NCHINI IZRAELI KWA MATIBABU YA MOYO


Watoto wanaokwenda nchini Israel kwa matibabu ya matatizo mbalimbali ya moyo kwa msaada wa taasisi ya Save the Children Heart  wakiwa na Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto Dk. Godwin Godfrey pamoja na wauguzi na wazazi wao.
Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) leo inasafirisha watoto nane kwenda nchini Israel kwaajili ya matibabu,  watoto hao ni wenye matatizo mbalimbali ya moyo ambapo   imeelezwa kwamba kati ya watoto milioni 1. 5 wanaozaliwa kwa mwaka,  asilimia 0. 9 wanazaliwa na matatizo ya moyo jambo ambalo taasisi hiyo haiwezi kumudu kuwatibu wagonjwa wote.


WAZAZI WATAKIWA KUUNGA MKONO MAPAMBANO DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA

 Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Stanley Mkandawile akizungumza na baadhi ya viongozi wa Jumuia hiyo kutoka katika Kata mbalimbali za wilaya ya Ilala, alipokutana nao katika kikao maalum cha kujitambulisha kwao, kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Ilala. Kulia ni Katibu wa Jumuia hiyo wilaya ya Ilala, Lugano Mwafongo. 

Akizungumza kwenye kikao hicho, pamoja na mambo mbalimbali Mkandawile ameitaka Jumuia ya Wazazi katika mkoa wake na maeneo mengine nchini, kuunga mkono hatua ya serikali kuingia katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

Mkandawile amesema, Kama sehemu ya Wanana CCM, Jumuia hiyo haiba budi kuunga mkono mabambano hayo kwa kuwa Serikali inatekeleza ilani ya CCM, ibaraya 118 hadi 119.
Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Stanley Mkandawile akiwasili ukumbini. Kushoto ni Katibu wa Jumuia hiyo wilaya ya Ilala, Lugano Mwafongo na kulia ni Katibu wa Jimbo la Ilala Christopher Lugemalila.
 Wajumbe wakiwa ukumbini. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.


UTAFITI: WANANCHI WENGI WAMEKUMBWA NA NJAA KATIKA KIPINDI CHA MIEZI MITATU ILIYOPITA

IDADI kubwa ya wahojiwa wa Sauti za Wananchi (asilimia 78) wameripoti uhaba wa chakula katika maeneo wanayoishi. Hali ni mbaya zaidi katika maeneo ya vijijini ambako asilimia 84 wameripoti uhaba wa chakula ikilinganishwa na asilimia 64 katika maeneo ya mijini.

Zaidi ya nusu ya kaya za Tanzania (yaani asilimia 69) zinahofia kuishiwa chakula. Aidha asilimia 51 ya kaya zimeripoti kwamba hakukua na chakula cha kutosha kulisha kaya nzima,  au mwanakaya ameshinda na njaa kwa sababu hakuweza kupata chakula (asilimia 50).

Matokeo haya yalitolewa na Twaweza katika muhtasari  uitwao Uchungu wa njaa: Upungufu wa chakula Tanzania. Muhtasari huu umetokana na takwimu za Sauti za Wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika wenye uwakilishi wa kitaifa unaotumia njia ya simu. 

Takwimu za muhtasari huu zimekusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,800 wa Tanzania bara (Zanzibar haikuhusishwa kwenye matokeo haya) kati ya Septemba 14 na 26, 2016 na kutoka kwa wahojiwa 1,610 kati ya Februari  9 na 15, 2017.

Kwa mujibu wa wananchi wengi, uhakika wa kupata chakula umepungua kati ya Septemba 2016 na Februai 2017: Februai 2017, asilimia 65 ya wananchi walikuwa na hofu ya kaya zao kukosa chakula cha kutosha ikilinganishwa na asilimia 45 waliosema hivyo mwezi Septemba 2016. Mwezi Februari 2017, asilimia 51 ya wananchi waliripoti kwamba kuna wakati hawakua na chakula cha kutosha kwa ajili ya kaya zao katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita. Kabla ya hapo, mnamo mwezi Septemba 2016, asilimia 43 ya wananchi iliripoti kwamba hali kama hiyo iliwatokea katika kipindi cha miezi kumi na miwili iliyopita. 

Mwezi Februari 2017, asilimia 35 ya wananchi waliripoti kuwa na mwanakaya angalau mmoja alieshinda na njaa siku nzima kwa sababu ya kukosa chakula katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita. Hili ni ongezeko kutoka asilimia 21 walioripoti kwamba hali hiyo iliwatokea katika kipindi cha miezi sita tangu Aprili mpaka Septemba 2016.

Takwimu za Benki Kuu ya Tanzania zinaonesha kwamba bei ya mahindi (halisi, jumla) imeongezeka mara mbili (baada ya kuirekebisha na kiwango cha mfumuko wa bei wa wakati huo) katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kutoka shilingi 400 kwa kilo mwanzoni mwa 2015 mpaka shilingi 852 mwezi wa kumi na mbili, 2016. Wahojiwa wa Sauti za Wananchi wameripoti kwamba kwa wastani kilo moja ya mahindi inawagharimu shilingi 1,253. (Bei zilizoripotiwa kwenye masoko ya ndani).

Upungufu na uhaba wa chakula unaoendelea ni kielelezo cha hali ngumu ya maisha iliyopo na umasikini wa kipato. Jumla ya watu nane kati ya kumi (asilimia 80) wameripoti kwamba kaya zao hazina kipato cha kutosha kukidhi mahitaji yao ya kila siku.
 
Aidan Eyakuze, Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza anasema: “Wananchi wamekumbwa vikali na upungufu wa chakula. Tumepokea mwitikio wa serikali katika suala hili na tunaunga mkono jitihada za kuzuia maafa makubwa. Hata hivyo, takwimu zinaonesha kwamba wananchi bado wanaishi kwenye hali ngumu na wamejaa hofu ya kukosa chakula. Jitihada za kuhakikisha kuwa hakuna Mtanzania yeyote anayelala njaa zishike nafasi ya kwanza  katika vipaumbele vyetu vya kitaifa.”


RAIS DKT. MAGUFULI ASALI IBADA YA JUMATANO YA MAJIVU KATIKA KANISA KATOLIKI LA MTAKATIFU PETRO OYSTERBAY JIJINI DAR ES SALAAM

Paroko Msaidizi wa Kanisa la Mtakatifu Petro Father Asis akimpaka majivu kichwani Rais Dkt. John Magufuli katika Ibada ya Jumatano ya Majivu iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokiya ya Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

 Paroko Msaidizi wa Kanisa la Mtakatifu Petro Father Asis akimpaka majivu kichwani Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamini Wiliam Mkapa katika Ibada hiyo ya Jumatano ya majivu.
 
 Paroko Msaidizi wa Kanisa la Mtakatifu Petro Father Asis akimpaka majivu kichwani Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli katika Ibada hiyo ya Jumatano ya majivu.


Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisali katika Ibada ya Jumatano ya Majivu pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamini Wiliam Mkapa, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli katika Kanisa Katoliki Parokia ya  Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

 Rais Dk John Magufuli na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa wakisalimiana na Masista wa Parokia ya Mt Petro wakati wa ibada ya jumatano ya Majivu.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisali katika Ibada ya Jumatano ya Majivu pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamini Wiliam Mkapa, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli katika Kanisa Katoliki Parokia ya  Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.



Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisali katika Ibada ya Jumatano ya Majivu pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamini Wiliam Mkapa, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli katika Kanisa Katoliki Parokia ya  Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.


Rais Dkt. John Magufuli akizungumza jambo na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa mara baada ya Ibada hiyo ya jumatano ya Majivu iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es Salaam.


AFRICA JOB CENTER KUWANUFAISHA WATANZANIA KATIKA KUPATA AJIRA


Msemaji wa Kampuni ya Africa Job Center, Doris Godfrey, akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu fursa za ajira zinazopatikana kupitia kampuni hiyo. Kushoto ni Mwakilishi wa Idara ya Mauzo, Edga Soka.
 Msemaji wa Kampuni ya Africa Job Center, Doris Godfrey, akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu fursa za ajira zinazopatikana kupitia kampuni hiyo. Kushoto ni Mwakilishi wa Idara ya Mauzo, Edga Soka.
Ufafanuzi.
Na Mwandishi Wetu
VIJANA wametakiwa kutumia simu zao za mkononi kwa manufaa zaidi ikiwa ni pamoja na kujitafutia ajira kwa njia ya mtandao.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi,Msemaji wa kampuni ya Africa Job Center (AJC) ambayo inawasaidia watu mbalimbali kupata kazi barani Afrika alisema teknolojia imerahisisha vitu hivyo ni rahisi kufuatilia na kujua kinachoendelea.

Alisema  wameamua kuwa kampuni ya vijana wa kitanzania ambao wanakazi ya kuwaunganisha wanaotafuta ajira na waajiri kutoka nchi tofauti ikiwa ni pamoja na Kenya, Burundi, Malawi na Rwanda.

“ Mtu anaweza kupata kazi  kwa kupitia mtandao na simu yake ya mkononi kwani unaweza kuwasiliana na muajiri moja kwa moja kupitia tuvuti yetu nakujipatia ajira”. alisema.
Alisema nafasi za kazi zilizopo katika tovuti yao ni kwanzia ngazi ya chini kabisa ya kufagia paka ngazi ya juu, ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara wanaweza kutoa matangazo yao.

Pia alisema kutakuwa na matamasha mbalimbali ya kuhamasisha watu wasio na ajira kutambua kuwa wanaweza kupata ajira nje ya Tanzania. www.africajobcenter.com