Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Sunday 13 October 2019

MIAKA SABA YA UTEKELEZAJI WA SERIKALI MTANDAO

 Ukurasa wa kuingia (log in page wa Mfumo Shirikishi wa Kusimamia Raslimali za Taasisi 
 UVUMBUZI wa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) umeleta fursa za maendeleo kwa mtu binafsi au kwa taasisi husika na faida nyingi zisizomithilika katika uendeshaji na utekelezaji wa shughuli mbalimbali na maisha kwa ujumla TEHAMA imekuwa ni njia mbadala ya kuhudumia wananchi na inapotumiwa na taasisi za umma katika utekelezaji wa shughuli zake na katika kuwahudumia wananchi kwa ufanisi na kwa gharama nafuu ndiyo hujulika kama serikali mtandao.

Hivyo, Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha inapata faida zitokanazo na matumizi ya TEHAMA kwa ufanisi, iliamua kuundaa taasisi mpya ambayo ilipewa majukumu ya kuratibu na kusimamia matumizi sahihi ya TEHAMA katika taasisi za umma ili ziweze kunufaika ipasavyo katika kuboresha utendaji kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hivyo, kwa kuzingatia hili Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora, Mh. Kapt. (Mst) George H. Mkuchika (Mb), anasema Serikali ilianzisha Wakala ya Serikali Mtandao iliundwa kwa mujibu wa sheria Na. 30, Sura ya 245 ya mwaka 1997 chini ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ikuwa na jukumu la kusimamia serikali mtandao na kuratibu maendeleo ya TEHAMA ndani ya Serikali na taasisi zake, baada ya kupitia matokeo ya tathmini ya hali halisi ya matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma za serikali ambapo taasisi nyingi zilionyesha kujitengenezea mifumo na raslimali nyingine za TEHAMA bila kujali uwepo wa jitihata hizo katika taasisi nyingine. Hali hiyo ilichochea kuwa na urudufu wa jitihata za TEHAMA zinazofanana na zisizowasiliana wala kubadilishana taarifa.

Akizungumzia hali ilivyokuwa kabla ya Serikali kujikita katika matumizi ya TEHAMA katika utoaji huduma kwa umma, Mhe. Waziri anaelezea kuwa, Serikali mtandao ni nyenzo inayotumika katika kubadili na kuboresha utendaji kazi katika taasisi za umma na utoaji wa huduma kwa wananchi. “Kazi hii sio rahisi kuifanikisha, inahitaji rasilimali za kutosha, utashi wa kisiasa, watumishi waliobadilika kimtazamo na kimatendo ili kuhakikisha serikali mtandao inatumika ipasavyo ndani ya Serikali na taasisi zake (G2G), kati ya Serikali na sekta ya biashara (G2B) na kati ya Serikali na wananchi (G2C). Ili kuyafikia yote haya, tunahitaji kubadili mifumo ya utendaji katika Serikali kwa ujumla”.

Naye Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais, Manejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora, Bw. Priscus anasema kuwa mwananchi anapata manufaa mengi kutokana na matumizi ya TEHAMA kwa kuwa anarahisishiwa upataji wa huduma mbalimbali hapo alipo bila kutembea umbali mrefu na kwa gharama nafuu. Kwa upande wa taasisi za umma, TEHAMA inarahisisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi katika kuhudumia wananchi wengi zaidi kwa wakati mmoja kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao Dkt Bakari Bakari akiongea  kuhusu jitihata za utekelezaji wa  Serikali Mtandao - UDOM Dodoma hivi karibuni
Akizungumzia mafanikio ya serikali mtandao yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwa Wakala ya Serikali Mtandao mwaka 2012 hadi sasa, Mtendaji Mkuu wa Wakala, Dkt. Jabiri Bakari anaeleza kuwa Serikali imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa serikali mtandao, husan katika maeneo ya sera, sheria na miongozo, usimamizi, utengenezaji wa mifumo tumizi na ya kimkakati ya TEHAMA, na ujenzi wa miundombinu ya pamoja ya TEHAMA. BOFYA HAPA KUONA ZAIDI


Wednesday 20 June 2018

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA AWAONYA WANASIASA



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU  WAJIBU WA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA KUTII SHERIA ZA NCHI ILI KUKUZA DEMOKRASIA NA AMANI YA NCHI
 
Nachukua fursa hii kuwaasa Viongozi wote wa Vyama vya Siasa na wanachama kutekeleza majukumu yao ya kisiasa kwa kufuata na kuzingatia Sheria na Kanuni za Vyama vya Siasa na Sheria za nchi kwa ujumla.

Kufuatia tabia iliyojitokeza ya baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Siasa nchini kutumia vibaya vyombo vya habari, hususani mitandao ya kijamii kufanya vitendo au kutoa kauli ambazo zinavunja sheria za nchi, ni wito wangu kwao kuacha tabia hiyo mara moja.

Ninasisitiza kuwa Viongozi wa Vyama vya Siasa wasitumie vibaya dhana ya demokrasia na uhuru wa habari, kuvunja Sheria za nchi. Ieleweke kwamba mtu yeyote anapokiuka sheria za nchi, Sheria itachukua mkondo wake bila kujali wadhifa wa mhusika katika chama cha siasa.

Rai yangu kwa Viongozi wote wa Vyama vya Siasa na wanachama wote wa vyama vya siasa nchini, ni wajibu wa kila mmoja wao kuelewa kwamba katika kutekeleza majukumu yao ya kisiasa wanapaswa kuheshimu Sheria za nchi wakati wote ili kudumisha na kukuza demokrasia ya vyama vingi nchini. Kwa kufanya hivyo pia, Viongozi hawa watalinda na kuimarisha Amani ya nchi yetu.

 
  Jaji Francis S.K. Mutungi
MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA


WAZIRI LUKUVI ATENGUA UTEUZI WA MCHECHU NHC


TAARIFA NZIMA YA WAZIRI MPINA KUHUSU KUKAMATWA KWA SAMAKI BUNGENI HII HAPA

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akitoa taarifa ya serikali kuhusu tukio la kukamatwa kwa samaki wachanga wasioruhusiwa kisheria katika mgahawa wa Bunge Juni 19,2018.


Thursday 14 June 2018

HII HAPA HOTUBA YA BAJETI YA SERIKALI 2018/2019

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango akionesha mkoba ulio na nyaraka za Bajeti ya serikali ya 2018/2019


Monday 11 June 2018

SERIKALI: HAKUNA MFUKO MAALUM WA KUHIFADHI FEDHA ZA KULIPA DENI LA TAIFA

Na Benny Mwaipaja, Dodoma
Serikali imesema kuwa hakuna akiba ya fedha iliyowekwa katika mfuko maalum kwa ajili ya kulipia Deni la Taifa kwa sababu deni hilo linajumlisha Deni la Serikali na Deni la Sekta Binafsi, lakini Serikali inalipa deni lake pekee bila kuhusisha deni la Sekta Binafsi.

Hayo yameelezwa Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji alipokuwa Akijibu maswali ya Mbunge wa Mtambile Mhe. Masoud Abdallah Salim aliyetaka kujua Deni la Taifa limefikia kiasi gani na namna mchanganuo wa fedha zilizowekwa akiba kwa ajili ya kulipa deni hilo ulivyo.

“Fedha kwa ajili ya malipo ya Deni la Serikali inatengwa kwa kuzingatia taratibu za kawaida za kibajeti kupitia Fungu 22, katika Mwaka wa Fedha 2017/18, Serikali ilitenga kiasi cha Sh. trilioni 1.262 kwa ajili ya malipo ya deni la ndani na Sh. bilioni 685.06 kwa deni la nje”, alisema Dkt. Kijaji.

Alisema hadi kufikia Aprili 30, mwaka huu Deni la Taifa limefikia Dola za Marekani milioni 26,161.02 sawa na zaidi ya Shilingi trilioni 59.4

Akijibu swali la nyongeza la Mbunge huyo aliyetaka kujua mkakati wa Serikali kuhakikisha Deni la Taifa linahakikiwa ili kujua kama Serikali inakopesheka au la, Dkt. Kijaji alilihakikishia Bunge kuwa kuanzia mwaka ujao wa fedha, Deni la Taifa litahakikiwa kama nchi nyingine zinavyofanya kwani mkataba wa kuhakiki deni hilo upo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika hatua za mwisho.

Waziri huyo alisema kuwa Deni la Taifa ni himilivu na Serikali imekuwa makini katika ulipaji kwa kuhakikisha inalipa kila mwezi madeni katika Taasisi zote ilizokopa hali inayoifanya nchi kuaminika na Taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa

Aidha, Mhe. Kijaji alifafanua kuwa fedha zote zinazokopwa zinapelekwa katika shughuli za maendeleo ya kiuchumi ili kuendelea kuinua uchumi wa nchi hususani katika kipindi hiki cha uchumi wa viwanda.


Tuesday 5 June 2018

RAIS MAGUFULI AWAAPISHA MAJAJI WATATU IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Jaji Ferdinand Wambali kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Jaji Mwanaisha Athuman Kwariko kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, Ikulu jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi kuwa Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania.


Majaji watatu walioapishwa wakila Kiapo cha Maadili Ikulu jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani Jaji Ferdinand Wambali akifatiwa na Jaji Mwanaisha Athuman pamoja na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi 


Majaji pamoja na watendaji wa Mahakama Kuu pamoja na Mahakama ya Rufani wakifatilia tukio la uapisho wa Majaji watatu Ikulu jijini Dar es Salaam.


Jaji wa Mahakama ya Rufani Jaji Ferdinand Wambali akizungumza mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Majaji watatu aliowaapisha Ikulu jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi, Jaji wa Mahakama ya Rufani Jaji Ferdinand Wambali pamoja na Jaji Jaji Mwanaisha Athuman Kwariko mara baada ya tukio la uapisho Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
x


MUKTASARI WA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA MWAKA 2018/19

Waziri wa Fedha na Mipango. Dk. Philip Mpango


BUNGENI JIJINI DODOMA LEO

WANAFUNZI wa Kidato cha Tano wa Shule ya Sekondari ya Tusiime ya Jijini Dar es Salaam wakiwa Bungeni jijini Dodoma jana kwa ziara ya kimafunzo. Ambapo walishuhudia shughuli mbalimbali za Bunge na namna Bunge linavyofanya kazi. Picha;Mroki Mroki/Daily News Digital-Dodoma

WANAFUNZI wa Kidato cha Tano wa Shule ya Sekondari ya Tusiime ya Jijini Dar es Salaam wakiwa Bungeni jijini Dodoma jana kwa ziara ya kimafunzo. Ambapo walishuhudia shughuli mbalimbali za Bunge na namna Bunge linavyofanya kazi.
WANAFUNZI wa Kidato cha Tano wa Shule ya Sekondari ya Tusiime ya Jijini Dar es Salaam wakiwa Bungeni jijini Dodoma jana kwa ziara ya kimafunzo. Ambapo walishuhudia shughuli mbalimbali za Bunge na namna Bunge linavyofanya kazi.
Wanachuo kutoka Chuo cha Usafirishaji Tanzania (NIT) wakiwa Bungeni kwa ziara ya kimafunzo.


Wanachuo kutoka Chuo cha Usafirishaji Tanzania (NIT) wakiwa Bungeni kwa ziara ya kimafunzo.


WANAFUNZI wa shule ya Mt Everist ya Jijini Dar es Salaam wakiwa Bungeni jijini Dodoma jana kwa ziara ya kimafunzo. Ambapo walishuhudia shughuli mbalimbali za Bunge na namna Bunge linavyofanya kazi.

WANAFUNZI wa shule ya Mt Everist ya Jijini Dar es Salaam wakiwa Bungeni jijini Dodoma jana kwa ziara ya kimafunzo. Ambapo walishuhudia shughuli mbalimbali za Bunge na namna Bunge linavyofanya kazi.

WANAFUNZI wa Kidato cha Tano wa Shule ya Sekondari ya Tusiime ya Jijini Dar es Salaam wakiwa Bungeni jijini Dodoma jana kwa ziara ya kimafunzo. Ambapo walishuhudia shughuli mbalimbali za Bunge na namna Bunge linavyofanya kazi.


WANAFUNZI wa Kidato cha Tano wa Shule ya Sekondari ya Tusiime ya Jijini Dar es Salaam wakiwa Bungeni jijini Dodoma jana kwa ziara ya kimafunzo. Ambapo walishuhudia shughuli mbalimbali za Bunge na namna Bunge linavyofanya kazi.


Maofisa mbalimbali kutoka Wizara ya Fedha na Taasisi zake wakiwa Bungeni jijini Dodoma wakati Bajeti ya Wizara yao ikisomwa na kujadiliwa.


SERIKALI YATOLEA UFAFANUZI WA MAFAO YA WATUMISHI KABLA YA PSPF

Na Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma
Serikali imesema kuwa watumishi wote wa Serikali Kuu walioajiriwa na kuthibitishwa katika ajira ya masharti ya kudumu na pensheni, kabla ya mwaka 1999 waliunganishwa katika Mfuko wa Pensheni wa PSPF kwa mujibu wa Sheria.

Hayo yameelezwa Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango,  Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum,  Lucy Mlowe aliyetaka kujua Serikali inawafikiriaje watumishi wa Sekta ya Afya walioajiriwa na Serikali Kuu miaka ya 1980 ambao fedha zao hazikukatwa na mfuko wa hifadhi ya jamii.

Dkt. Kijaji, alisema kuwa Kabla ya Julai 1999 mfumo wa malipo ya mafao ya kustaafu kwa watumishi wa Serikali Kuu haukuwa wa kuchangia hivyo watumishi wote waliokuwa kwenye ajira ya masharti ya kudumu wanastahili malipo ya uzeeni wakiwemo watumishi wa Sekta ya Afya hata bila kuchangia.

“Kwa mujibu wa Ibara ya 5 ya Sheria ya Mfuko wa Pensheni wa PSPF, watumishi wote wa Serikali Kuu ambao waliajiriwa na kuthibitishwa katika ajira ya masharti ya kudumu na pensheni wanakuwa wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF kuanzia tarehe ya kuanzishwa kwa mfuko”, alisema Dkt. Kijaji.

Alisema kwa mujibu wa Sheria ya Mafao ya Hitimisho la Kazi Na. 2 ya mwaka 1999 kwa watumishi wa umma ambayo ilianzisha Mfuko wa Pensheni wa PSPF, wastaafu wote ambao ni wanachama wa Mfuko huo na wanaguswa na sheria hii wanalipwa mafao ya kustaafu na mfuko huo kwa kipindi chao chote cha utumishi.

Dkt. Kijaji alibainisha kuwa mafao ya watumishi yanakokotolewa kuanzia tarehe ya kuajiriwa hadi wanapostaafu utumishi wao kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma.


Tuesday 29 May 2018

WIZARA YA ARDHI YAOMBA BILIONI 73 KWA MWAKA 2018/2019.

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maedeleo ya Makazi, Willium Lukuvi akiwasilisha Bungeni hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi kwa wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo ameliomba Bunge kujadili na kuopitisha kiasi cha shilingi 73,071,273,632 iloi wizara iweze kutumiza majukumu yake.
 Waziri, Lukuvi ameliambia Bunge kuwa katika mwaka wa fedha wa 2018/19 wizara inataraji kukusanya kiasi cha Shilingi Bilioni 120 kutokana na kodi, tozo, na ada mbalimbali za zinazotokana na shughuli za sekta ya ardhi kwa kutekeleza mikakati ambayo wamejiwekea. 
 Msemaji wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi na Maliasili na Utalii, Halima Bulembo akisoma taarifa ya Kamati Bungeni leo.
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi akijadili jambo na Naibu Waziri wake, Dk. Angelina Mabula Bungeni leo. 
 Wabunge wakiwa Bungeni jijini Dodoma leo 
 Wageni wakiwa Bungeni jijini Dodoma
 Wabunge Munira Mustapha akijadili jambo na Hussein Bashe Bungeni jijini Dodoma.
 Wageni wakiwa Bungeni wakifuatulia kikao cha Bunge leo. BOFA HAPA KUONA ZAIDI.


Monday 28 May 2018

SIMANZI YA TAWALA BUNGENI, KIFO CHA MBUNGE KASUKU BILAGO

 VILIO, Majonzi na Simanzi vimetawala katika viunga vya Bunge jijini Dodoma hii leo kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Buyungu, Mwalimu Kasuku Bilago. Anaandika Mroki Mroki – Daily News Digital, Dodoma

Mwalimu Bilago alifikwa na umauti wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jumamosi Mei 26, mwaka huu  jijini Dar es Salaam.
 Muda mfupi baada ya Naibu Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson kufungua kikao cha Bunge kwa kusoma dua, alitoa Bungeni hapo Taarifa ya Spika kuhusiana na msiba huo mzito uliolifika Bunge, naabade kutangaza kuahirisha Bunge hadi Mei 29 saa tatu asubuhi, ili kupisha Maombolezo huku mipango ya kuuleta mwili katika viwanja vya Bunge kwa heshima za mwisho ikifanyika.
 Daily News Digital ilishuhudia wabunge wakitoka Bungeni huku wakiwa na nyuso za huzuni na wengi wao wakibubujikwa na machozi na vilio vya kwikwi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amemtaja marehemu kuwa ni miongoni mwa wabunge Bora ambao walikuwa wakijenga hoja  na kutoa michango yenye maslahi mapana kwa Jimbo lake na nchi kwa ujumla.

Nae Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule alizungumzia msiba huo na kusema ni pengo kubwa Mwalimu Bilago ameliacha si kwa Kambi ya Upinzani bali kwa Bunge zima kutokana na mchango wake aliokuwa akiutoa.
 “Mwalimu Bilago alikuwa Mwalimu kweli kweli, hakuna siku ambayo alisimama kuchangia asipate sapoti ya Bunge zima nah ii ni kutokana na ucheshi wake lakini pia hoja zake za msingi alizokuwa akizitoa Bungeni,”alisema Haule.

Mwili wa Marehemu Bilago unataraji kuletwa Bungeni Mei 29 kwa heshima za mwisho na baade kusafirishwa hadi Kijiji cha Kasuga Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ambako utahifadhiwa Mei 30 mwaka huu. 
 Wabunge mbalimbali wakifarijiana kufuatia Msiba huo mzito wa Mwezao.
 Mawaziri wakiweka saini katika kitabu cha maombolezo cha Mbunge Kasuku Bilago wa Jimbo la Buyungu, Wilayani Kakonko mkoa wa Kigoma.
Wabunge wakisaini kitabu cha maombolezo