Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Wednesday 31 May 2017

WAZIRI MKUU AHIMIZA UJENZI WA NYUMBA ZA BEI NAFUU

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama picha za nyumba wakati alipotembelea Maonyesho ya Mpango wa ujenzi wa Nyumba za Gharama Nafuu kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma  Mei 30, 2017. Maonyesho hayo yameandaliwa na Muungano wa  Vikundi Vya Vicoba Tanzania (VIGUTA) .Kushoto  ni  Mwenyekiti wa Taifa wa VIGUTA, Dkt. Salmin Ibrahim Dauda.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezitaka Halmashauri za wilaya nchini ziangalie uwezekano wa kuwapatia watumishi wake nyumba za bei nafuu kwa malipo kidogo kidogo.

Amesema Halmashauri za wilaya kupitia mapato ya ndani, japo si makubwa zinaweza kuandaa mazingira yatakayowawezesha watumishi wake kupata nyumba kupitia mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu unaofanywa na Muungano wa Vikundi vya Vicoba Tanzania (VIGUTA).

Ametoa wito huo leo (Jumatano, Mei 31, 2017) mara baada ya kutembelea maonyesho ya Mpango wa Ujenzi wa Nyumba za Waheshimiwa Wabunge (Low Cost Housing) yanayoendelea kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma. 
         
Waziri Mkuu aliwashauri  viongozi wa VIGUTA wafanye mawasiliano na Halmashauri zote na akawataka watenge muda wa kuzitembelea  Halmashauri hizo ili kuonyesha nia na uwezo wao wa kujenga nyumba za gharama nafuu ambazo malipo yake hulipwa kidogo kidogo kwa lengo la kuboresha maisha ya Watanzania.

“Watanzania wengi hivi sasa wanapendelea nyumba ndogo, nzuri na ambazo zimekamilika. “Wengi wao, na hasa wafanyakazi, siku hizi wana shughuli nyingi na hawana muda wa kujenga nyumba na kuzisimamia wenyewe kama zamani. Hivyo, wanahitaji makampuni yanayoweza kuwanjengea nyumba na wao wakalipa kidogo kidogo,” amesisitiza.
         
Aliwaaasa viongozi wa VIGUTA wahakikishe kuwa wanajenga nyumba zenye ubora unaokubalika ili waweze kuaminika hali ambayo itawawezesha kupata wateja wengi zaidi.

“Katika kipindi hiki ambacho Serikali inahamia Dodoma, Muungano wa Vikundi vya VICOBA au VIGUTA unayo nafasi kubwa ya kuwapatia watumishi wanaohamia nyumba za kuishi kupitia mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu,” Waziri Mkuu alisema.

Alisema watumishi wengi wanaoingia gharama kubwa kwa kuishi katika nyumba za kupanga huku wakilipa kodi, sasa wamepata kimbilio kwani  wanaweza kujengewa nyumba kwa muda mfupi na kwa bei nafuu na wakalipa kidogokidogo kwa kipindi cha hadi miaka 15.

Naye, Mwenyekiti wa VIGUTA Taifa, Dkt. Salmin Ibrahim Dauda alimweleza Waziri Mkuu kwamba wana uwezo wa kujenga nyumba kwa gharama ya shilingi milioni 12, milioni 15, milioni 25 na milioni 60 kutegemeana na ukubwa wa nyumba.

Alisema wameweka viwango tofauti ili kuwawezesha Watanzania wenye kipato cha chini kumiliki nyumba zao wenyewe.


RAIS MAGUFULI AMLILIA MZEE NDESAMBURO



Marehemu Mzee Philemon Ndesamburo (kulia) akiwa na Mbunge wa jimbo la Ubungo, Saed Kubenea wakizungumza jambo wakati wa Mkutano baraza Kuu la Chadema uliofanyika mjini Dodoma Mei 27,2017. 

“Kwa masikitiko nimepokea taarifa za kifo cha Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Moshi Mjini, Mzee wangu Philemon Ndesamburo kilichotokea leo tarehe 31 Mei, 2017 katika hospitali ya rufaa ya KCMC iliyopo Moshi Mkoani Kilimanjaro, Namkumbuka Mzee Ndesamburo kwa hekima zake na uongozi wake uliozingatia siasa za kistaarabu”

Hii ni kauli ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa katika salamu zake za rambirambi kwa familia ya Marehemu Philemon Ndesamburo, Viongozi na wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wote walioguswa na kifo hicho.

Mhe. Rais Magufuli amesema alifanya kazi na Marehemu Philemon Ndesamburo wakati wote wakiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wakati wote walishirikiana, kutaniana na anamkumbuka kwa namna ambavyo alitumia muda wake bungeni kupigania mambo yenye maslai kwa wananchi wa jimbo lake la Moshi Mjini.

Mhe. Dkt. Magufuli ameitaka familia ya Marehemu Philemon Ndesamburo na wote waliguswa na msiba huu kuwa na moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu na amemuombea Marehemu apumzishwe mahali pema peponi, Amina.


Tuesday 30 May 2017

OFA KWA WATANZANIA KUTEMBELEA HIFADHI ZA WANYAMAPORI




MARA MWENYEJI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI



Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dk Charles Mlingwa, akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Mara hii leo kuhusiana na mkoa huo kuwa mwenyeji wa siku ya mazingira.
 ****************
MKOA wa mara umechaguliwa kuwa mwenyeji wa Siku ya mazingira duniani ambapo kitaifa itaadhimishwa kitaifa mkoa wa Mara katika Wilaya ya Butiama kuanzia Juni 1-6 mwaka huu.

Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Januari Makamba anataraji kufungua maadhimisho hayo na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan anataraji kuwa mgeni rasmi katika kilele chake.

Maadhimisho hayo yatafanyika katika uwanja wa Mwenge Mjini Butiama ambapo kutakuwapo na kongamano na tafrija mbalimbali kuhusiana na maswala ya mazingira.

Mkuu wa mkoa wa Mara, Dk Charles Mlingwa alisema kuwa katika siku hiyo ya mazingira inategemewa kupandwa miche ya asili 1,500 ya miti katika misitu mbalimbali eneo la Butiama kama ilivyo kawaida ya maadhimisho hayo.

Aidha Dk Mlingwa amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi ili kujumuika pamoja kwenye maadhimisho hayo muhimu ambayo yatafanyika mkoani Mara kwa mara ya kwanza.

Mbali na hapo Mlingwa alisema kuwa wananchi watapata faida katika maadhimisho hayo kama kuijengea jamii uwezo juu ya uelewa wa masuala ya mazingira na changamoto za kijamii zinazojitokeza katika utunzaji wa mazingira na kuwezesha wadau kushiriki katika fursa zinazohusiana na upandaji wa miti.

Pia watapata fursa ya kujadili mwendelezo wa utekelezaji wa shughuli zilizoratibiwa katika mkoa na wizara kuhusu namna bora ya uhifadhi wa mazingira na kuenzi kazi zote za Baba wa Taifa Mwal. Julius Nyereree katika hifadhi ya mazingira.

Mlingwa alisema kuwa wataelimishwa kupanda miti ili kukidhi mahitaji ya dunia ya kupambana na ongezeko la hewa ya ukaa.

Kaulimbiu ya mwaka huu ni “Hifadhi mazingira muhimili wa Tanzania ya viwanda” ikiwa na maana ya ulinzi na uhifadhi wa mazingira nchini kuleta maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.


UPEPO MKALI WA KASI YA KILOMETA 40 KWA SAA WATARAJIWA KUVUMA PWANI YA TANZANIA

UPEPO mkali wa kusi wenye kasi ya kilometa 40 kwa saa unataraji kuvuma utasababisha mawimbi yenye ukubwa wa mita 2 baharini.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania imetoa tahadhari ya kuwepo kwa upepo huo mkali na mawimbi makubwa katika maeneo ya pwani ya Tanzania.

Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba huko Kisiwani Zanzibar ndivyo vitakubwa zaidi na upepo huo.

"Msukumo wa upepo wa Kusi unatokana na kuimarika kwa mgandamizo mkubwa wa hewa katika ukanda wa pwani ya Tanzania," Ilisema taarifa ya TMA.

Tahadhari kubnwa imetolewa kwa wavuvi na watumiaji wengine wa bahari hasa maeneo yaliyotajwa ili kuepuka ajali ambazo zinaweza kuepukika.

Hali hiyo ya hewa inatarajiwa kuwepo hadi kufikia kesho 31 Mei,2017.


GREEN WASTEPRO LTD WANG'ARISHA BUSTANI YA ASKARI MONUMENT

 Bustani ambayo imehifadhi historia ya vita kuu ya kwanza ya dunia (1914-1918)ikiwa na Sanamu ya askari Mwafrika katika sare ya kijeshi ya King's African Rifles aliyeshika bunduki yenye kisu cha kando na kutazama upande wa bahari, imefanyiwa ukarabati mkubwa na Kampuni ya kizalendo ya Green Waste Pro Ltd. Kampuni hiyo kama sehemu ya kurejesha faida kwa jamii ilitengeneza bustani hiyo iliyozinduliwa jana kwa gharama zake wakisimamiwa na mamlaka husika za wilaya na halmashauri. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa bustani hiyo iliyofungwa kwa muda mrefu kwa ajili ya ukarabati kwenye msafara wa mbio za Mwenge, Meneja Msaidizi wa Green WastePro, Erick Mark alisema wamefurahi kwa mwenge kuzindua bustani hiyo inayorembesha mji na kuufanya uwe nadhifu
Muonekano wa bustani ya Askari monument kabla ya kuzinduliwa rasmi.

Sanamu hiyo iliyowekwa 1927 na Waingereza kama kumbukumbu ya askari na wapagazi Waafrika waliopigana vita Afrika ya Mashariki iliyomuondoa Mjerumani, iliondoa sanamu ya mtawala wa kijerumani Hermann VonWissman iliyowekwa mwaka 1911.
Eneo hilo ambalo sasa lina muonekano unaong'aa zaidi kutokana na kazi iliyofanywa na kampuni hiyo, ni sehemu ya kampeni kubwa ya kampuni ya Green WastePro Ltd iliyoanzishwa mwaka 2011 ikiwa na lengo la kusaidia halmshauri ya manispaa ya Ilala kuwa safi, ya kushawishi wakazi wa Dar kuupenda mji wao na kuusaidia kuuweka bora. Akifafanua zaidi kuhusu mradi wa upendezeshaji bustani ya sanamu ya askari maarufu kama Askari Monument, Mark alisema kazi waliyofanya ni kushawishi watanzania kutambua umuhimu wa usafi na kuringia kuwa na jiji safi hasa katikati ya Jiji.  Kiongozi wa mbio za mwenge, Amour Hamad Amour akiwa ameshika mwenge baada ya kufika mtaa wa Posta Mpya jijini Dar kwenye uzinduzi wa bustani ya Askari Monument katika manispaa ya Ilala iliyokarabatiwa na kampuni ya Green WastePro ltd.

Alisema wanakazi kubwa ya kukabiliana na changamoto za ongezeko la takataka na udhibiti wa uchafuzi wa mazingira hususani hapa katikati ya jiji la Dar es salaam kwenye kitovu cha taifa, kazi ambayo wao wamekuwa wakifanya kwa ufanisi mkubwa usiku na mchana, bila kuchoka toka mwaka 2012 walipopewa dhamana hiyo na Halmashauri ya manispaa ya Ilala kwa mara ya kwanza.

Mbali na kazi hiyo pia wamekuwa wakijihusisha na shughuli mbalimbali za kijamii kwa utaratibu wa kujitolea (Corporate Social Responsibility) kama vile upandaji wa miti, utoaji wa vifaa vya kuhifadhia taka mashuleni, usafishaji wa fukwe, utoaji wa vifaa vya kuhifadhia taka na utunzaji wa mazingira maeneo mbalimbali ya jiji letu la Dar es Salaam hususani kwenye Halmashauri yetu ya Manispaa ya Ilala. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.


KIFAA CHA DIJITALI KUWAWEZESHA WAKULIMA WADOGO TANZANIA KUPATA FEDHA, PEMBEJEO NA MAFUNZO

Mwakilishi wa AGRA nchini, Bw. Vianey Rweyendela akifafanua jambo wakati wa uzinduzi huo.
  Uzinduzi ukifanywa na Mkuu wa AGRA nchini Bw. Vianey Rweyendela (wa pili kulia) kwa kushirikiana na wawakilishi wa Positive International Limited (PIL), na Grameen Foundation.
Wakulima wadogo nchini Tanzania hivi karibuni wataweza kupata taarifa mbalimbali za kijiditali kuhusu masuala ya pembejeo, ukiwemo ushauri utakaosaidia kutatua matatizo yanayowakabili kama vile upatikanaji wa fedha, pembejeo na mafunzo. 

Mradi huo umezinduliwa na taasisi tatu za Alliance for a Green Revolution in Africa (AGRA), Positive International Limited (PIL), na Grameen Foundation katika sherehe zilizohudhuriwa na maofisa wa serikali, wawakilishi wa vyama vya wakulima, taasisi za fedha, kampuni za mbegu, wafanyabiashara wa nyenzo za kilimo na wale wanaojishughulisha na biashara za mazao ya sekta ya kilimo.  BOFYA HAPA KUONA ZAIDI.


MATUKIO MBALIMBALI KWENYE MAONYESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA JIJINI TANGA

Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akitoa elimu kuhusu umuhimu wa wananchi kujiunga na mfuko huo kwa wakazi wa Jiji la Tanga kwenye banda lao lililopo katika eneo la Mwahako Jijini Tanga kunakofanyika maonyesho ya tano ya biashara ya kimataifa
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage akiptia kwenye banda la Hifadhi za Taifa Tanzania (Tanapa) wakati alipofungua maonyesho ya kimataifa ya  biashara ya tano yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage akisalimiana na mmoja wa watumishi Tanapa wakati wakati alipotembelea banda lao kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage akiendelea na shughuli ya kukagua mabanda ya Maonyesho
Afisa Habari za Utalii (TTB William Akile kulia akiongeza na baadhi ya wanafunzi waliotembelea banda lao
 Afisa Habari za Utalii (TTB William Akile kulia akiongeza na baadhi ya wanafunzi waliotembelea banda lao
 Afisa Habari za Utalii (TTB William Akile kulia akiongeza na baadhi ya wanafunzi waliotembelea banda lao
 Maafisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wakitoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Tanga katika Banda lao lililopo kwenye eneo la Mwahako Jijini Tanga kunapofanyika Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Tano kutoka kushoto ni Msimamizi wa Ofisi ya Mfuko wa Bima ya Taifa Mkoani Tanga (NHIF) Dinna Mlwilo katikati ni Sabrina Komba ambaye ni Afisa Masoko na Elimu kwa umma makao makuu na kulia ni Afisa matekelezo Macrina Clemens
 kulia ni Sabrina Komba ambaye ni Afisa Masoko na Elimu kwa umma makao makuu Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kulia ni Afisa matekelezo Macrina Clemens wakimsikiliza kwa umakini mkazi wa Jiji la Tanga ambaye alifika kwenye banda lao kupata ufafanuzi kuhusu huduma zinazotolewa na mfuko huo
 Afisa matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Macrina Clemens kulia akisitiza jambo kwa mkazi wa Jiji la Tanga kuhusu umuhimu wa kujiunga na mfuko huo ili kuweza kunufaika na huduma mbalimbali muhimu ikiwemo za matibabu kushoto ni Meneja wa Mfuko huo Mkoani Tanga,Ally Mwakababu katikati ni  Msimamizi wa Ofisi ya Mfuko wa Bima ya Taifa Mkoani Tanga (NHIF) Dinna Mlwilo kulia kwake ni Afisa Masoko na Elimu kwa umma makao makuu Sabrina Komba

 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akiwa na maafisa wengine wa mfuko huo wakiwa tayari kutoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Tanga kuhusu namna wanavyoweza kunufaika kupitia mfuko huo
 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akitoa elimu kwa mkazi wa Jiji la Tanga ambaye alitembelea banda lao
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda lao kuhusu faida za wakazi wa Jiji la Tanga kujiunga na mfuko huo lakini pia namna walivyojiandaa na ujio wa mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga. Source: Tanga Raha Blog.


RC GAMBO AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUACHA DHANA YA KUOGOPA KUSTAAFU

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akizungumza katika mkutano wa nane wa wadau wa mfuko wa mafao ya kustaafu wa GEPF jijini Arusha juzi ,wakati akifunga mkutano huo ambapo aliwataka wastaafu watarajiwa kujiandaa kustaafu kwa kubuni miradi mbalimbali ya kuongeza kipato hali itakayosaidia wao kujiendeleza kimaisha(Habari Picha na Pamela Mollel Arusha)
 Katibu Mkuu katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Eric Shitindi akizungumza katika mkutano huo ambapo alisema ni vyema watumishi wakajianda mapema wakiwemo wa umma na sekta binafsi
Mkurugenzi wa mfuko wa GEPF Daudi Msangi alisema kuwa tayari kuna mikakati mbalimbali ambayo imeletwa kwenye mkutano huo na itaanza kufanyiwa kazi kwa malengo ya kuboresha maslai ya wanachama na nchi kwa ujumla
Mwenyekiti wa bodi Ya wadhamini,wa mfuko huo Joyce shaidi akizungumza katika mkutano huo
 Kulia ni mkuu wa kitengo cha kusimamia amana za wawekezaji katika benki ya CRDB Bw.Masumai Ahmed

Wadau wa mkutano wakiwa wamesimama kuashiria kumalizika kwa mkutano huo
******************
Mkuu wa mkoa  wa arusha Mrisho Gambo amewataka Watumishi katika sekta za umma  kuacha dhana ya kuogopa  kustaafu kazi pindi wanapofikia muda wa kustaafu badala yake wanatakiwa kujipanga kabla muda haujafika.

Aidha watumishi wanaogopa kustaafu kwa kuwa wanaanza kujiandaa miaka miwili kabla hali ambayo inawapa uoga mkubwa wastaafu watarajiwa

Mrisho Gambo ameyasema hayo jana  wakati akifunga mkutano wa mfuko wa mafao ya kustaafu (GEPF) uliokuwa ukiendelea  jijini Arusha

Gambo alisema kuwa kwa sasa wastaafu wanapata magonjwa ya moyo kwa kuwa hawajajiandaa na kubuni miradi ambayo inaweza kuwaletea vipato kama mishahara yao ilivyokuwa

Alisema maandalizi ni muimu sana kwa wafanyakazi hata kama bado hawajafikia muda wa kustaafu kwani kustaafu sio ajali bali ni kitu ambacho kipo na kimeshawekewa utaratibu na mifuko ya hifadhi jamii hapa nchini pamoja na Serikali.

"Wastaafu wengi wanakufa pindi wanapoacha kazi hiyo sio sawa ni lazima kila mtu ajiandae na abuni njia mojawapo ya kujiongezea kipato kwani hata kama ukijiajiri mwenyewe ni lazima utapata kipato kama kile ulicho kuwa unalipwa kama sehemu ya ujira wako "aliongeza Gambo.

Wakati huo huo aliwataka wakuu wa mifuko ya hifadhi hapa nchini kuhakikisha kuwa wanatoa elimu ya kujiandaa kustaafu kwa wafanyakazi wake kwani uzoefu unaonesha kuwa asilimia kubwa ya wafanyakazi hawana elimu hiyo

Alisema kama wafanyakazi watakuwa na elimu hiyo ya kustaafu basi itasaidia kupunguza  ulalamishi kwa wastaafu,magonjwa ya moyo,vifo visivyo na lazima vinavyotokea.

Naye mkurugenzi wa mfuko huo Daudi Msangi alisema kuwa tayari kuna mikakati mbalimbali ambayo imeletwa kwenye mkutano huo na itaanza kufanyiwa kazi kwa malengo ya kuboresha maslai ya wanachama na nchi kwa ujumla.