Rais
wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino (aliyevaa shuka la
kimasai) akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania Leodger
Tenga mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius
Nyerere (JNICC) tayari kwa kikao cha shirikisho hilo mapema hii leo jijini Dar
es Salaam.
Baadhi
ya Wajumbe wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) wakiwasili katika Kituo
cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) tayari kwa kikao cha
shirikisho hilo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya Wajumbe wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) wakiangalia bidhaa
mbalimbali za uchongaji na ushonaji toka kwa wajasiriamali wa Tanzania kabla ya
kuanza kwa kikao cha shirikisho hilo mapema hii leo katika Kituo cha Kimataifa
cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.
Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino (katikati)
akiwasili katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) tayari
kwa kikao cha shirikisho hilo mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni
Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika Ahmad Ahmad na kulia ni Rais wa
Shirikisho la Soka Tanzania Wallace Karia.
Rais
wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino (aliyevaa shuka la
kimasai) akivalishwa urembo wa mkononi wenye rangi za bendera ya Taifa mara
baada ya kuwasili katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere
(JNICC) tayari kwa kikao cha shirikisho hilo mapema hii leo jijini Dar es
Salaam.
Afisa
Uhusiano Mkuu toka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Geofrey Tengeneza (kushoto)
akimkabidhi Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino,
zawadi mbalimbali toka bodi hiyo kabla ya kuanza kwa mkutano wa shirikisho hilo
mapema hii leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere
(JNICC), jijini Dar es Salaam. Picha
na Idara ya Habari - MAELEZO
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment