Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday 22 February 2018

RAIS WA FIFA AKIWA NCHINI TANZANIA LEO

Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino (aliyevaa shuka la kimasai) akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania Leodger Tenga mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) tayari kwa kikao cha shirikisho hilo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wajumbe wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) wakiwasili katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) tayari kwa kikao cha shirikisho hilo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wajumbe wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) wakiangalia bidhaa mbalimbali za uchongaji na ushonaji toka kwa wajasiriamali wa Tanzania kabla ya kuanza kwa kikao cha shirikisho hilo mapema hii leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino (katikati) akiwasili katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) tayari kwa kikao cha shirikisho hilo mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika Ahmad Ahmad na kulia ni Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania Wallace Karia.
Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino (aliyevaa shuka la kimasai) akivalishwa urembo wa mkononi wenye rangi za bendera ya Taifa mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) tayari kwa kikao cha shirikisho hilo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.

Afisa Uhusiano Mkuu toka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Geofrey Tengeneza (kushoto) akimkabidhi Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino, zawadi mbalimbali toka bodi hiyo kabla ya kuanza kwa mkutano wa shirikisho hilo mapema hii leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam. Picha na Idara ya Habari - MAELEZO


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment