Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 23 February 2018

HAKUNA KUCHUKUA MAENEO BILA KULIPA FIDIA –NAIBU WAZIRI ANGELINA MABULA


Naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Angelina mabula akiwa katika ziara yake mkoani Mara.
Naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Angelina mabula akizungumza na watumishi wa halmashauri za Mji na Wilaya ya musoma mkoa wa Mara.
Naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Angelina mabula akikagua mfumo wa ukusanyaji kodi ya ardhi katika halmashauri ya manispaa ya Musoma mkoa wa Mara.
Baadhi ya watumishi wa halmashauri ya manispaa ya Musoma wakimsikiliza Naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Angelina mabula wakati wa ziara yake mkoa wa Mara. (Picha na WANMM)
**************
Na Mwamdishi Maalum – Musoma
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Mkazi Angelina Mabula amesema ni marufuku halmashauri kuchukua maeneo ya wananchi bila ya kuwalipa fidia.
 
Mabula amesema hayo Wilayani Butiama mkoa Mara wakati wa ziara yake yenye nia ya kutatua migogoro ya ardhi pamoja na kukagua mfumo wa ukusanyaji kodi ya ardhi.

Amesema wakati wa mchakato wa kuchukua maeneo ya mwananchi ni vyema wahusika wakashirikishwa kuanzia hatua ya awali sambambana na kuelimishwa juu ya zoezi hilo ili kuepuka migogoro inayoweza kutokea.

‘’cha msingi ni kuanza kuzungumza na mwananchi kabla ya kuchukua eneo lake na kumueleza eneo ambalo ataachiwa na halmashauri zihakikishe mwananchi huyo anapimiwa pamoja na kupatiwa hati yake’’ alisema Mabula

Aidha,  Mabula amesema eneo litakalochukuliwa na halmashauri viwanja vyake kuuzwa fedha itakayopatikana halmashauri ihakikishe inatumika katika kutengeneza miundo mbinu na huduma nyingine za jamii na kusisitiza kuwa kwa kufanya hivyo migogoro haiwezi kutokea.

Naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi ameziagiza halmashauri kuhakikisha zinapanga miji kulingana na ‘master plan’ ili kuwa miji bora iliyopangika


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment