Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Sunday 13 August 2017

MWAKYEMBE: NINAMATUMAINI MAKUBWA NA VIONGOZI WAPYA WA TFF

 WAZIRI wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harson Mwakwyembeakizungumza baada ya viongozi wapya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupatikana katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Mjini Dodoma Agosti 12,2018.

Viongozi wapya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Rais TFF, Wallace Karia (kulia) akiwa na Makamu wa Rais wa Shirikisho hilo, Michael Wambura wakimsikiliza Waziri mwenye dhamana ya Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, baada ya kutangazwa washindi wa Uchaguzi wa TFF uliofanyika mjini Dodoma Agosti 12,2017.
 *****************
WAZIRI wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Harson Mwakwyembe aliwapongeza wajumbe kwa kufanya uchaguzi wa kistaarabu na hatimaye kuwapata viongozi wapya wa kuliongoza Shirikisho hilo kwa miaka minne.

Pia Mwakyembe alitoa shukrani zake kwa wajumbe kutoka CAF na FIFA, kwa ukaribu wao waliouonyesha tangu mwanzo wa mchakato wa uchaguzi mbaka kufiki jana ambapo ndiyo ilikuwa mwisho.

“Kwakweli nawashukuru watu wote ikiwemo wajumbe wa CAF na FIFA kutokana na ushirikiano wao mkubwa katika ucahguzi huu, lakini nawapongeza sana wagombe walioshindwa na walioshinda kwasababu kwenye uchaguzi kuna mambo mawili kupata na kukosa hivyo nilazima kukubali na kitu cha msingi naomba wale walioshindwa kuwaunga mkono wenzao ili waweze kufanya kazi ya kujenga mpira wa Tanzania kwa pamoja,”alisema Mwakyembe.

Waziri huyo wa michezo alisema anamatumaini makubwa na viongozi wapya waliochaguliwa kwani kazi kubwa iliyopo mbele yao ni kuhakikisha soka la Tanzania linasonga mbele na kuanzia mwakani anataka viongozi hao wawajibike kutoa taarifa ya misada wanayopata kutoka FIFA kwenye magazeti.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment