Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Sunday 4 March 2018

NAIBU SPIKA TULIA ATOA MSAADA TAASISI ZA DINI MBEYA

 NAIBU Spika Dk.Tulia Ackson ameshiriki ibada takatifu katika kanisa la Jerusalem Temple Sokomatola, Mjini Mbeya ambapo pamoja na kushiriki na waumini wenzake katika ibada hiyo Dk Tulia pia alitoa jumla ya shilingi milioni mbili na laki tano kama msaada wake ikiwa Milioni moja kwa  ajili ya sikukuu ya wakinamama, Milioni moja na nusu alinunua CD mbili za kwaya katika kanisa hilo.
Dk. Tulia akifanyiwa maombi maalum.
Pia Dk Tulia alipata fursa ya kushiriki kama mgeni rasmi kwenye  Maulid ya wanawake wa kiislam mkoa wa Mbeya iliyofanyika katika msikiti wa Masjid Fyii Sabili Ilah uliopo Forest ambapo alitoa msaada wa vitabu vya mafundisho ya kiislam na Quran tukufu pamoja na kulipia huduma zote ikiwemo chakula.
"Sisi kama viongozi yawezekana wakati mwingine tukawa hatuwafikii kwa wakati watumishi wa dini lakini mara zote tupo pamoja nanyi na tunatambua sana mchango wenu katika taifa kwa maombi yenu na haswa katika kuwalewa watoto wetu katika maadili mema ambayo yatasaidia kuwa na raia wazuri wenye kumcha Mungu," Dk Tulia.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment