Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Sunday 7 January 2018

SERIKALI YAMFUNGIA PRETTY KIND MIEZI SITA KUFANYA SANAA

Mwanadada Suzan Michael 'Pretty Kind' aliyeimba limbo wa VIDUDUWASHA ambaye leo semrikali imemfungia kujihusisha na sanaa kwa miezi sita. 
Na Mwandishi wetu.
SERIKALI imemfungia msanii Suzan Michael ‘Pretty Kind’ kujihusisha na sanaa kwa kipindi cha miezi sita.

Akitangaza uamuzi huo leo jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza amesema uamuzi huo ni kutokana na msanii huyo kutoa wimbo wa “VIDUDUWASHA” aliyomshirikisha msanii mwenzake Gift Stanford ‘Gigy Money, ambao haufuati maadili ya kitanzania.

Aidha msanii huyo imebainika kuwa anafanya kazi ya Sanaa bila kusajiliwa na Baraza la Sanaa la Taifa, pamoja na kuweka mtandaoni picha ya nusu utupu kinyume na maadili ya Kitanzania.

“Kumekuwa na wimbi kubwa la wasanii sasa hivi kutoa nyimbo zenye maneno ya matusi na zisizo na maadili pamoja na wasanii hasa wanawake kupiga picha wakiwa wamevaa nusu utupu na kuweka picha hizo katika mitandao,nataka kuwapa angalizo wasanii wenye tabia hizi kuwa Serikali inawafuatilia kwa karibu na mwaka huu tumeanza na huyu na wengine wanafuata,”alisema Shonza.

Miongoni mwa wasanii ambao wametajwa kuwa miongoni mwa wanaokiuka maadili na kuchafua sanaa ya Tanzania ni pamoja na mwana dada, Gift Stanford ‘Gigy Money’ na  Jane Rimoy ‘Sanchi’ ambao nao wakati wowote watakumbwa na mkono wa sharia.

Shonza amemtaka msanii Gigy Money kufika ofisini kwake haraka, huku akionya kuwa msanii huyo hawezi kushindana na Serikali.

Nae Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA),Godfrey Mngereza  amesema kwa mujibu wa Kanuni  31 (1) ya Baraza ya mwaka 2005,inaeleza kuwa msanii kufanya kazi bila kusajiliwa ni kosa na anaweza kufungiwa, na pia kwa upande wa mavazi zinasema msanii anatakiwa kuvaa mavazi yenye staha yasiyomdhalilisha wala kudhalilisha watazamaji wake. 

“Napenda kuwasisitiza wasanii wote ambao wanajijua kuwa hawajasajiliwa BASATA kuja kujisajili haraka na kwa wale waandaji wa kazi za Sanaa kama waongozaji , (Directors),Waandaaji (Producers) na wamiliki wa Studio za kurekodi kazi za Sanaa  ambao hawajasajiliwa nao waje kujisajili haraka”, amesema Mngereza.

Msanii Suzan Michael ‘Pretty Kind’ aliomba radhi mashabiki wake kwa kufanya makosa hayo pamoja na watanzania wote kwa ujumla na kuaahidi kujirekebisha na kuto kurudia tena makosa hayo.

Naibu waziri Shonza ametoa rai kwa  wamiliki wa vyombo vya Habari kutokubali kupiga nyimbo au video za wasanii zisizo na maadili kwani  wanakuwa ni sehemu ya kutangaza vitendo hivyo vilivyo kinyume na maadili  kwani itafika mahali serikali itachukulia hatua hata vyombo vinavyopiga nyimbo zisizo na maadili.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment