Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 9 January 2018

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI MKUU MSTAAFU EDWARD LOWASSA IKULU

Rais Dkt. John Magufuli akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais  Dkt. John  Magufuli akifurahia jambo na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Rais  Dkt. John Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya kumaliza mazungumzo yake na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 Rais Dkt. John   Magufuli akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
**********
Rais Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 09 Januari, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Ngoyai Lowassa, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Baada ya mazungumzo hayo, Edward Ngoyai Lowassa amempongeza Rais Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya na ametaja baadhi ya maeneo ambayo kazi kubwa imefanyika kuwa ni kutoa elimu bila malipo, ujenzi wa mradi wa uzalishaji wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge), ujenzi wa viwanda na ujenzi wa reli kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) ambavyo vinazalisha ajira nyingi kwa Watanzania.

“Nimepata faraja sana kuja hapa Ikulu kuonana na Mhe. Rais, tumezungumza nae na nimempongeza kwa kazi nzuri anayoifanya, lazima tukiri anafanya kazi nzuri na anahitaji kutiwa moyo.


“Moja kubwa ambalo ni la msingi sana ni la kujenga ajira, katika kuanza ujenzi wa reli ya kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro hapo anajenga ajira, na kwenye nchi yoyote inayoendelea suala muhimu ni kujenga ajira, Stiegler;s Gorge ni kujenga ajira na mingine ya aina hiyo, lazima kuwepo na kipaumbele cha kusema kwamba tunajenga ajira, jingine ni la elimu, ni muhimu sana, hauwezi kuacha elimu katika mambo yako unayofanya, hili nalo lazima lisemwe vya kutosha, kwa kweli nakushukuru Mhe. Rais, you made my dayamesema Lowassa.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment