Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 3 November 2017

WAWILI WAFA AJALINI WAKIWAHI KESI MAHAKAMANI ARUSHA

Gari dogo aina ya Toyota Mark X T 796 DFG walilokuwa wakisafiria David Chijana (33) aliyekuwa akiendesha gari hilo na James Alfed (40) wakazi wa Dar es Salaam.
 Gari baada ya kupata ajali.
WATU wawili wamekufa papo hapo baada ya gari walilokuwa wakisafiria Toyota Mark X T  namba za usajili  T 796 DFG kupata ajali USA River jijini Arusha leo mchana. Anaandika Mroki Mroki.

Mashuhuda wa ajali hiyo wanasema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva aliyekuwa akiendesha gari hiyo inayosemekana ilikuwa ikitokea dar es Salaam kwenda jijini Arusha.

Mmoja wa waliopoteza maisha ni David Chijana Karani wa Idara ya Ufundi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

Aidha taarifa za awali zinasema kuwa marehemu Chijana aliondoka jijini Dar es Salaam jana jioni kwenda Arusha kuhudhuria kesi ya mirathi.

Chanzo kingione kinasema kuwa David alikuwa akiwahi Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ambapo mama yake alikuwa mmoja wa watuhumiwa waliokuwa wakisomewa hukumu ya kesi ya Wizi Benki ya Exim ambapo hata hivyo alikuhukumiwa kwenda jela miaka mitano.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha,  Charles Mkumbo amethibisha kutokea kwa vifo hivyo na kuwataja marehemu kuwa ni David Chijana (33) aliyekuwa akiendesha gari hilo na James Alfed (40) wote wakazi wa Dar es Salaam.

 Kamanda Mkumbo alisema chanzo cha gari hilo ni mwendo kasi ambapo kabla ya ajali iligongana na gari aina ya Noah kasha kuruka juu  na kusababisha vifo katika eneo la River Tree Kata ya Pori kwenye barabara ya Moshi /Arusha na ilitokea  saa 4:35 asubuhi.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment