Home
About Us
Siasa
Uchumi
Biashara
Michezo
Burudani
Wasiliana Nasi
Have you got a good story?
Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.
Have you got a good story?
Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.
Saturday, 6 May 2017
NEC YATOA UFAFANUZI UTARATIBU WA KUMPATA MBUNGE NA DIWANI VITI MAALUM
Saturday, May 06, 2017
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeeleza kuwa nafasi za Wabunge wa Viti Maalum wanaoteuliwa zipo kwa mujibu wa Sheria na zimeainishwa katika Ibara ya 78 (1) na (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.
Akitoa ufafanuzi huo leo jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani amesema kuwa Ibara ya 78 (1) na (4) ya Katiba inaeleza utaratibu mzima wa kuwapata Wabunge wanawake wa Viti maalum.
Amesema kila Chama cha Siasa kinachoshiriki katika Uchaguzi Mkuu na kupata angalau asilimia 5 ya Kura zote halali za wabunge kitapata Wabunge wa Viti Maalum kulingana na Kura ambazo chama husika kimepata.
Amefafanua kuwa Chama kinachopata asilimia 5 ya Kura zote halali za Wabunge katika Uchaguzi Mkuu kinatakiwa kuwasilisha orodha ya wanachama wanaopendekezwa kuwa wagombea wa Viti Maalum ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Aidha, ameeleza kuwa endapo inatokea nafasi wazi ya Mbunge wa Viti Maalum katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokana na sababu mbalimbali, Spika wa Bunge humtaarifu Mwenyekiti wa Tume juu ya uwepo wa nafasi hiyo kwa mujibu wa kifungu cha 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343.
Amesema kuwa Mwenyekiti wa Tume hukiandikia barua chama husika kukitaarifu juu ya uwepo wa nafasi wazi ya viti maalum ili kiweze kuwasilisha pendekezo la jina katika orodha kiliyowasilishwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi mwaka 2015, ikiambatanishwa na Fomu namba 8 D ya kuomba jina lililopendekezwa liteuliwe na Tume katika nafasi ya Ubunge kulingana na sifa zilizoainishwa kwa mujibu wa Sheria.
Saturday, May 06, 2017
Copyright: Dailynews Blog
Mtumie Rafiki Yako
Maoni: 0
Email This
BlogThis!
Share to X
Share to Facebook
Newer Post
Older Post
Home
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
Tags
Kumbu Kumbu
MAKONDA AWAONGEZEA NGUVU TBC
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo ametoa msaada wa Gari aina ya Noah,Pikipiki Tatu, Komputer Tano na Camera Mbili za kisasa kw...
WAZIRI MKUU APOKEA TAARIFA YA KAMATI INAYOSGHULIKIA MGOGORO WA LOLIONDO
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (kulia)leo 2 February 2017 akionyesha Kitabu cha Taarifa ya Kamati inayoshughulikia Mgogoro wa Loliondo ...
MAJINA YA WANAFUNZI WA SHULE YA ST LUCK VICENT YA ARUSHA WALIOFARIKI YATAJWA
Majina ya wanafunzi 29 wa Shule Lucky Vicent ya jijini Arusha waliokuwa katika ziara ya kimafunzo kuelekea Ngorongoro wakitumia basi a...
KANALI NDAGALA ATEKETEZA BANGI HEKA NNE ILIYOLIMWA NDANI YA PORI LA AKIBA KIGOSI
Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma, Kanali Hosea Ndagala (mwenye kombati) akisaidia kupanga kuni kwaajili ya kutekeza bangi ili...
KAJEMBE; MZARAMO ALIYEUTEKA MJI WA MOSHI KWA BIASHARA YA KUKAANGA MIHOGO
WAANDISHI wa Habari ni watu wa kuzunbuka sana nchini na Duniani kwa ujumla katika harakati za utafutaji habari za kuhabarisha jamii juu ...
TBA WAPEWA SIKU 3 WAWE WAMEMALIZA UBOMOAJI JENGO LA TANESCO UBUNGO
KATIBU Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Nyamhanga ameipa siku tatu Wakala wa Nyumba ch...
TAARIFA NZIMA YA WAZIRI MPINA KUHUSU KUKAMATWA KWA SAMAKI BUNGENI HII HAPA
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akitoa taarifa ya serikali kuhusu tukio la kukamatwa kwa samaki wachanga wasioruhusiwa kisheria k...
PASIPOTI MPYA NI SALAMA ASILIMIA 100: UHAMIAJI
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini, Dkt. Anna Makakala akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. Na Mwandishi Wet...
WAZIRI MKUU AAGIZA UJENZI WA MAABARA UKAMILISHWE HARAKA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza hii leo wakati wa kuzindua rasmi usambazaji wa vifaa mbalimbali vya maabara za Sayansi katika sh...
TAARIFA YA SERIKALI KUHUSU UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CHAMA CHA MAPINDUZI YA MWAKA 2015 - 2020
HOTUBA YA MHE. KASSIM M. MAJALIWA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AKIWASILISHA TAARIFA YA SERIKALI KUHUSU UTEKELEZAJI ...
Labels
BURUDANI
MICHEZO
SIASA
Kumbu Kumbu
January
(86)
February
(95)
March
(131)
April
(117)
May
(113)
June
(127)
July
(81)
August
(69)
September
(46)
October
(55)
November
(21)
December
(47)
January
(66)
February
(32)
March
(41)
April
(40)
May
(27)
June
(9)
October
(1)
BLOG MBALI MBALI
Father Kidevu
USHIRIKI WA WANANCHI WAIMARISHA UPANDAJI MITI SAO HILL
MICHUZI BLOG
KIHONGOSI AFANYA KIKAO KAZI NA VIONGOZI,WASANII BENDI YA TOT
HABARI LEO
Arusha on spotlight
OFA YA MATANGAZO
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment