Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday 24 August 2017

SPIKA NDUGAI KUANIKA RIPOTI YA UCHUNGUZI WA MAUZO YA VITO VYA TANZANITE NA ALMASI WIKI IJAYO

BOFYA VIDEO HIYO KUMSIKILIZA SPIKA WA BUNGE

SPIKA wa Bunge, Job Ndugai amesema kuwa wiki ijayo atatoa taarifa kuhusu  kazi zilizofanywa na  kamati mbili  za wabunge wanaochunguza mwenendo mzima wa makinikia na madini ya vito ili kuona namna madini hayo yanavyonufaisha Watanzania. Anaandika Francisca Emmanuel

Amesema kuwa licha ya kuwapa siku 30, kamati hizo bado zinaendelea na kazi na kwamba zilitembelea maeneo ya machimbo ya madini ikiwemo Merelani kufanya uchunguzi wa kina.  

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Ndugai alisema kuwa bunge lililopita la bajeti aliunda kamati mbili muhimu kufuatilia masuala ya makinikia na madini kwa ujumla hususani ya dhahabu  na kuongeza kamati ya vito (almasi na Tanzanite) zenye wajumbe 11 kila moja.

‘’Kwa kuwa sikuwepo nchini kwa wiki kadhaa, itakuwa ni mapema sana kusema  chochote lakini kuanzia kesho kutwa ambapo nitakwenda Dodoma kupata mrejesho wa shughuli nzima zimeendeleaje lakini taarifa nilizonazo kamati zimefanya kazi nzuri sana,’’alisema Ndugai.

Alifafanua kuwa wiki ijayo atatoa taarifa ya nini kitafuata kufuatia kazi za kamati hizo kwani shughuli kubwa imefanyikia Dodoma.

Hata hivyo, alisema kuwa kamati nyingine za Bajeti na masuala ya Ukimwi zimeanza vikao vyake na kwamba Jumatatu kamati zote za Bunge zitaanza vikao Dodoma


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment