Makamu wa Rais, Samia Suluhu
Hassan akihutubia wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Kuwawezesha Wanawake
Kiuchumi la mkoa wa Dar es Salaam
Makamu wa Rais Samia Sulihu Hassan akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema (katikati) na kushoto ni Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson.
Makamu wa Rais, Samia Suluhu
Hassan akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa Jukwaa la Kuwawezesha
Wanawake Kiuchumi wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Kuwawezesha Wanawake
Kiuchumi la mkoa wa Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais, Samia Suluhu
Hassan amewata wanawake wote washirikiane, wapendane na wasimame imara
kuhakikisha nafasi ya mwanamke inaheshimika.
Makamu wa Rais ameyasema hayo
wakati wa Uzinduzi wa Jukwaa la Kuwawezesha Wanawake Kiuchumi mkoa wa Dar Es
Salaam.
Katika mkutano huo
uliohudhuriwa na wanawake zaidi ya elfu tatu wa mkoa Dar Es Salaam, Mhe. Samia
alisema Jukwa lililozinduliwa leo ni jukwaa la 23 la mkoa kufunguliwa.
Alisema mwakam 2015 dunia
ilimaliza utekelezaji wa malengo 8 ya Milenia ambayo kulikuwa na lengo namba 3
linazungumzia usawa wa kijinsia kumwezesha mwanamke .
“Ni muhimu kuhakikisha kuwa ifikapo ukomo wa
utekelezaji wa Ajenda ya Malengo Endelevu mwaka 2030,usawa wa mwanamke utakuwa
umefikia asilimia 50 kwa 50 katika Nyanja zote ikiwemo ngazi ya maamuzi,”
alisema Samia.
alisema lengo kubwa la
kuanzisha majukwaa ya kumwezesha mwanamke kiuchumi nchini ni kuwaunganisha
wanawake na fursa za masoko, mikopo ya riba nafuu na elimu ya ujasiriamali pia
kubadilishana mawazo.
Alisisitiza “Ni vyema
pia kuhakikisha kuwa Majukwa haya yanakuwa na utaratibu wa kutembelewa ili
kuweza kubadilishana uzoefu na pia fursa zikitokea zisambazwe kote hususani
kwenye Majukwaa ya Vijijini ili kuhakikisha tunaenda mbele kwa pamoja. Miongoni
mwetu humu kuna wabobezi wa masuala mengi; hivyo mnaweza kujipanga
kubadilishana ‘experts’ na kuhakikisha kila Mwanamke Mtanzania ananufaika na
keki ya Watanzania.”
Kaulimbiu ya uzinduzi wa
jukwaa hilo ni “MWANAMKE TUMIA FURSA KUSHIRIKI UCHUMI WA VIWANDA”.
Wanawake wanaweza kujipanga na kuona namna gani wanaweza kujikomboa
kiuchumi na kuhakikisha kuwa wanashiriki kikamilifu katika kujenga Tanzania
mpya ya viwanda.
Samia alisema “Muda umefika
sasa, wa kuwakomboa wanawake kutoka katika utumwa na lindi la umaskini
linalotokana na kutowezeshwa kiuchumi, kuna umuhimu wa kuwapa ujuzi na maarifa;
kuwawezesha kupata mikopo yenye riba nafuu na kwa urahisi; kukamilisha
uanzishwaji wa programu ya utekelezaji ya kumwezesha mwanamke kupitia manunuzi
ya umma; kuweka mifumo ya kisheria itakayopiga vita mila kandamizi; kuondoa
vikwazo katika masoko; kuweka mifumo madhubuti ya kibenki na mifuko ya hifadhi
za jamii hasa hifadhi ya Afya ili kujikwamua kwenye umaskini.
Mwishio Makamu wa Rais alihimiza
katika kwa wanawake wengi kupata elimu ya ujasiriamali na elimu ya kulipa kodi
kwani kodi ni muhimu sana katika maendeleo ya Taifa.
Makamu wa Rais aliwashukuru
Benki ya CRDB kwa kuchangia jukwaa hilo kwa kutoa hundi ya shilingi milioni 20
na pia aliwashukuru wadau wengine walioshiriki katika kufanikisha mchakato wa
kuunda jukwaa hilo unakamilika.
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment