Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Monday 15 May 2017

WAZAZI WAJIBIKENI KATIKA MALEZI YA WATOTO WENU; UMMY MWALIMU

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana kuhusu maalum ya familia duniani iliyoadhimishwa jana ambapo kauli mbiu ni 'Elimu na Malezi Bora kwa Ustawi wa Watoto'. Kushoto ni  Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Watoto, Emmanuel Burton. (Picha na Mroki Mroki). 
 ****************
Na Halima Mlacha, Dodoma
KATIKA kuadhimisha Siku ya Familia Duniani, Serikali imewataka wazazi kuhakikisha wanawajibika ipasavyo katika malezi ya watoto wao, ili kuzuia jamii ya watanzania kuwa na watoto na vijana wanaojiingiza kwenye matumizi ya dawa na uhalifu.

Aidha, imewaomba viongozi wote wa dini nchini kuhakikisha wanatumia dakika chache katika mahubiri yao, kuzungumzia malezi bora ya watoto ili kupunguza kasi ya ukatili wa watoto na kuondokana na kizazi cha watoto watukutu na wahalifu.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana kuhusu maadhimisho hayo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alisema wizara hiyo imebaini pamoja na kuwepo kwa sababu nyingine zinazowafanya vijana kujiingiza kwenye uhalifu na matumizi ya dawa za kulevya, lakini ukosefu wa malezi bora ya wazazi au walezi nao pia unachangia.

 “Tunawaomba viongozi wa dini watumie japo dakika tatu kwenye kila mahubiri yao kuzungumzia malezi bora, tunaamini nguvu ya viongozi wa dini wakilisemea hili familia zitakuwa bora hali hii itasaidia sana kupunguza matatizo yanayowapata watoto wetu,” alisema Mwalimu.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment