Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Wednesday 19 April 2017

SERIKALI KUENDELEA NA UKARABATI WA NYUMBA ZA NHC



Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi  imesema kuwa Shirika la Nyumba nchini(NHC)  limeweka mkakati wa kuhakikisha nyumba zote zilizo katika hali ya uchakavu zinafanyiwa ukarabati mkubwa na zile ambazo kiwango cha uchakavu ni kikubwa zinavunjwa na kuendeleza upya viwanja hivyo.

Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula  amesema  Bungeni mjini Dodoma leo kuwa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeshafanya uhakiki wa nyumba zake zote na kubaini hali halisi ya kila nyumba na kuweka mpango wa kuzifanyia ukarabati nyumba hizo kwa awamu.

Amebainisha kuwa katika mwaka wa fedha 2016/17 shirika lilitenga takribani shilingi bilioni 11 kwa ajili ya kuzifanyia ukarabati nyumba zake ambapo hadi mwezi Machi, 2017 jumla ya nyumba 2451 zilikuwa zimekwishafanyiwa ukarabati kupitia bajeti hiyo.

Aidha amesema kuwa shirika hilo linatarajia kumaliza ukarabati wa nyumba zote katika mwaka wa fedha 2017/18 na kusisitiza kuwa matengenezo ya nyumba hizi ni kazi endelevu kwa shirika hivyo bajeti ya matengenezo itaendelea kutengwa kila mwaka ili wapangaji wa nyumba za shirika waendelee kuishi katika nyumba na mazingira bora.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment