Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 2 March 2018

SERIKALI YAOMBA USHIRIKIANO ZAIDI NA BENKI YA DUNIA ILI KUHARAKISHA MAENDELEO YA NCHI

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango akijadiliana jambo na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania, Bi. Bella Bird na Mkurugenzi wa Uchumi, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Felipe Jaramilo, mara baada ya kikao kilichofanyika Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Uchumi Jumla, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Felipe Jaramilo akifafanua jambo katika kikao na Waziri wa Fedha na Mipango kilichofanyika Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akizungumza na ujumbe wa Mkurugenzi wa Uchumi jumla, Biashara na Uwekezaji (hawapo pichani), katika kikao kilichofanyika Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 **********************
Na Benny Mwaipaja, WFM
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uchumi Mpana, Biashara na Uwekezaji wa Benki ya Dunia, Dkt. Felipe Jaramilo katika ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango Dar es Salaam.

Katika kikao hicho, Waziri wa Fedha na Mipango aliishukuru Benki ya Dunia kwa kuendelea kuisaidia Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Dk. John Pombe Joseph Magufuli katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maedeleo hapa nchini.

Dkt. Mpango ameeleza kuwa uchumi wa nchi umeendelea kukua kwa kiwango cha kati ya asilimia 6-7 kwa muda na hivyo kuiwezesha Serikali kuendelea na utoaji wa huduma za jamii na kuwekeza katika miradi mbalimbali ya maendeleo.

Dkt. Mpango ameeleza kuwa pomaja na nia ya kuendeleza mafanikio mazuri yaliyopatikana katika awamu za Serikali zilizopita, Serikali ya Awamu ya Tano ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli imedhamiria kwa dhati kujenga uchumi imara kwa kuendeleza viwanda na kuweka mazingira mazuri ya biashara ili kuvutia wawekezaji wa ndani na wale wa nje kuja kuwekeza nchini , kujenga miundombinu ya barabara, reli, umeme , viwanja vya ndege na kuongeza uwekezaji katika utoaji wa huduma za jamii kama vile elimu, afya na maji.

Aidha, ameeleza kuwa katika kufikia malengo hayo , Serikali imefanya juhudi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato, kusimamia vizuri matumizi ya fedha za Serikali, kuongeza bajeti ya maendeleo hadi kufikia asilimia kati ya 35 na 40 ya bajeti nzimat, kuongeza ufanisi katika utendaji wa umma na kupambana na rushwa pamoja na mambo mengine.

Pamoja na ukuaji mzuri wa uchumi, Dkt. Mpango alisema kuwa Taifa bado linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa ajira kwa vijana, kiwango cha umasikini bado kiko juu, ukuaji mdogo wa Sekta ya kilimo ambayo imeajiri takribani asilimia 70 ya watanzania unaosababishwa na ukosefu wa mbegu bora, miundombinu ya umwagiliaji na soko la uhakika, na kupungua kwa mikopo ya benki za biashara kwa sekta binafsi pamoja na mambo mengine.

Katika kusaidi juhudi za Serikali kupambana na changamoto mbalimbali , Dk. Mpango aliiomba Benki ya Dunia kupitia kwa Dk. Felipe kuisadia Serikali mkopo wa Dola za Kimarekani milioni 150 kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa uchumi na utoaji huduma ( Growth and Service Delivery) amabao uko katika hatua ya maandalizi.

Mkurugenzi wa Uchumi Mpana, Biashara na Uwekezaji wa Benki ya Dunia, Dkt. Felipe Jaramilo, kwa upande wake aliipongeza Serikali ya awamu ya tano ya Dk. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi nzuri inayofanya ya kusimamia uchumi mpana, kuongeza makusanyo ya ndani ambayo yanasaidia upatikana fedha kwa ajili ya kugharamia uwekezaji katika miradi mbalimbali ya maendeleo, kupambana na rushwa, kusimamia matumizi ya fedha za umma, na kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi za umma.

Aidha, Dkt. Felipe aliishauri Serikali kuwekeza zaidi katika rasilimali watu na miundombinu ili kulifanya Taifa kuweza kuhimili ushindani wa kimataifa dunia na kujenga uchumi unaokua na endelevu.

Vile vile aliieleza kuwa katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita uwekezaji kutoka nje umekuwa zaidi katika Sekta ya madini, hivyo alishauri Serikali kuweka mazingira mazuri ya biashara ili kuwavutia wawekezaji kutoka nje kuwekeza katika sekta za viwanda na utoaji huduma ili kuongeza wigo wa shughuli za kiuchumi na kuchochea ukuaji wake.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment