Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 2 February 2018

DK KILANGI ATEULIWA KUWA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

Rais Dkt John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Adelardus Kilangi (pichani) kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).
Taarifa iliyotolewa jioni hii na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. Adelardus Kilangi umeanza Februari 1, 2018.
Kabla ya uteuzi huu Dkt. Kilangi alikuwa Mkurugenzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (St. Augustine University) kituo cha Arusha, na pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (Tanzania Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA).
Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua, Paul Joel Ngwembe kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali (DAG) kuanzia leo Februari 1, 2018.
Kabla ya Uteuzi huu, Ngwembe alikuwa Mkurugenzi wa masuala ya sheria katika Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (Tanzania Insurance Regulatory Authority – TIRA).
Kufuatia uteuzi huu,Rais Magufuli amewateua aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Mcheche Masaju na aliyekuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Gerson Mdemu kuwa Majaji wa Mahakama Kuu kuanzia Februari 1, 2018.

Wateule wote wataapishwa Jumamosi Februari 03, 2018 saa 9:00 Alasiri.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment