Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Saturday 29 April 2017

MKUU WA MKOA WA MBEYA AWAONGOZA WAKAZI WA JIJI LA MBEYA KUFANYA USAFI SOKO LA WAMACHINGA NANENANE

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla (wapili kushoto) akishiriki kufanya usafi katika Soko jipya la Machinga lililoo nanenae jijini Mbeya leo.
Wananchi wakishiriki kufanya usafi.
Wafanyakazi wa Benki ya Akiba wakiwa na Mkoo wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla baada ya kufanya usafi.
Baadhi ya maofisa wa vyombo vya ulinzi na usalama walioshiriki katika kufanya usafi leo

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amewaongoza wakazi wa jiji la Mbeya kufanya usafi katika soko la wamachinga la Nanenane jijini humno leo.

Akizungumza wakati wa kufanya usafi Makalla amewahimiza wakazi wa Mbeya kuunga mkono kampeni ya kuliweka jiji la Mbeya na mkoa na halmashauri zote kuwa safi.

Aidha Makalla ameishukuru Benki ya Akiba kutoa msaada wa Vifaa vya usafi, na wafanyakazi wa Akiba Bank kushiriki kufanya usafi na Benki hiyo kukubali ombi lake  kutoa mikopo kwa wamachinga.

Meneja wa Akiba Tawi la Mbeya Amehaidi kukutana na wamachinga hao na wengine katika masoko maalum kwanza kuwapa Mafunzo na baadaye kuwapatia mikopo.

Mbali na Mkuu wa Mkoa na Wafanyakazi hao wa Benki pia viongozi wa vyama vya Siasa , vyombo vya ulinzi na usalama na wamachinga walijitokeza kufanya usafi katika soko la nanenane ambalo litakalofunguliwa hivi karibuni kwa ajili ya Machinga wapatao 1,500

Wakizungumza katika risala yao wamachinga wamemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwasaidia kujengwa kwa choo cha kisasa , kuwekwa umeme na Maji katika soko hilo na kuahidi kuhamia sokoni hapo ifikapo Julai mosi.

Mkuu wa Mkoa amemwagiza  Mkuu wa usalama barabarani na Sumatra kuweka kituo cha Daladala katika eneo hilo mapema wiki ijayo jambo ambalo wamachinga wamelipongeza kwani litachochea biashara


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment