Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 11 April 2017

MWANZA YAPANIA KUIPIKU DAR ES SALAAM KIUCHUMI



 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella (kushoto) akizungumza wakati wa ufunguzi wa jukwaa la Biashara jijini Mwanza hii leo Aprili 11,2017. Mongella katika hotuba yake alisema Mwanza inafursa mbalimbali za kiuchumi hivyo miaka michache ijayo anaamani kuwa Mwanza itashika usukani wa uchumi nchini na kuipiku Dar es Salaam.
 Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali (TSN) Dk Jim Yonazi akizungumza wakati wa Jukwaa la Biahara jijini Mwanza leo. TSN ndio waandaaji wa jukwaa hilo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza. Dk Yonazi amewaomba wadau mbali mbali wamuunge mkono mkuu wa mkoa John Mongela katika juhudi za fursa za kibiashara na kuongeza kuwa TSN ni watu wa vitendo na tunaendelea kutenda ili kuhakikisha wanatimiza malengo ya kampuni hiyo.


Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbasi akizungumza katika Jukwaa la Biashara jijini Mwanza na mutoa Siri sita za kumsaidia mtu kufanikiwa katika biashara.
 Meza kuu ikipiga picha na washariki wote.
 Baadhi ya washiriki.
Na Alexander Sanga,Mwanza
Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela ameahidi kuwa mkoa wake utakuja kuwa wa kwanza kitaifa katika kuwa na vitengo mbali mbali vya uwekezaji.

Akizungumza katika jukwaa malumu la biashara lilioandaliwa na kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Mongela alisema ni wakati wa mkoa huo kubadilika na kuzitumia ipasavyo fursa za kibiashara kwa manufaa ya sasa na badae.

Mongela alisema mkoa umetenga hekta 72 katika eneo la Nyamongolo na hekta 500 katika eneo la Lwanyima kwajili ya ujenzi wa viwanda kwa wadau watakaojitokeza katika uwekezaji huo.

Mkuu wa mkoa ameahidi kwa wadau watakaojitokeza watapewa maeneo kwa kufuata taratibu za kisheria ndani ya wiki moja tu.

“Tunalenga kupata maeneo mengi zaidi kwa uwekezaji na kurahisisha mchakato wa kuipata kwa ajili ya uwekezaji na mpaka sasa Pato la Taifa(GDP) ya  mkoa wetu sasa hivi ni shilingi 9.3trilion  na tunaenda kwa  kasi sana”Mongela alisema.

Mkuu wa mkoa alisema  shilingi bilioni 7.6 zimetolewa kwa ajili ya mnara wa kuongozea ndege ‘control tower’ itakayoonyesha  mpaka Sudan kusini.

“Ndani ya miaka miwili Mwanza itapiga hatua kubwa kwa miundombinu ya usafirishaji na viwanda vingi vinakuja na fursa kibao za uwekezaji na endapo Stanadard Gauge ikikamilika  mizigo ya Uganda itakuwa ikichukuliwa mkoani kwetu” Mongela alisema.

Pia Mongela aliahidi endapo uwanja wa ndege wa mkoani hapa ukikamilika ndege za kimataifa zitakuwa zikitua hapa.

Mkurugenzi mtendaji wa TSN, waandaaji wa Jukwaa hilo la Biashara jijini Mwanza, Dr Jim Yonazi amewaomba wadau mbali mbali wamuunge mkono mkuu wa mkoa John Mongela katika juhudi za fursa za kibiashara.

Dr Jim alisema kuwa TSN ni watu wa vitendo na tunaendelea kutenda ili kuhakikisha wanatimiza malengo ya kampuni hiyo.

“Mwanza itakuwa sehemu ya mikakati yetu na TSN itaendlea kutoa huduma za kuwafikia wadau wote mkoani hapa” Yonazi alisema.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment