Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 9 May 2017

MKUU WA WILAYA AHIMIZA UJENZI WA MAKTABA

 Baadhi ya kazi ya sanaa za wanafunzi wa shule ya sekondari Mtoni
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mary Tesha akipanda mti katika madhimisho ya miaka 10 ya shule ya sekondari Mtoni
 **************
Na Alexander Sanga,Mwanza
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mary Tesha amewaomba wananchi na wadau mbali mbali wajitokeze kwa wingi katika kuhakikisha wanachangia katika ujenzi wa maabara na jengo la utawala katika shule ya sekondari ya Mtoni.

Akizungumza katika madhimisho ya miaka kumi,tokea kuanzishwa kwa shule,Tesha amewaomba wananchi wa kata ya Mabatini wahakikishe wanachangia kwa wingi ili kuhakikisha ujenzi wa maabara na jengo la utawala linaanza mapema.

Tesha alimuagiza diwani wa kata ya Mabatini Deus Lucas ahakikisha anawahamasisha wakazi wa Mabatini wachangia katika ujenzi huo.Tesha alichangia shilingi milioni 1.

Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Mtoni Denis Mwakisimba alisema wanafunzi wa shuleni wanapata changamoto kubwa katika kujisomea kutokana na ukosefu wa maktaba.

Mwakisimba ameipongeza serikali ya awamu ya tano kwa kuleta vitabu 1200 vya masomo ya sayansi.Mwakisimba alilamikia kuwepo kwa soko katika eneo la shule jambo linalopelekea kuleta usumbufu wakati wanafunzi wakiwa masomoni.

Kwa mujibu wa Mwakisimba alisema mpaka kukamilika kwa ujenzi wa maktaba na madarasa jumla itagharimu shilingi milioni 250 Katika Harambe iliyofanyika shuleni hapo wakazi wa Mabatini walichangia milioni 1.8.

Wadau mbalimbali waliahidi mifuko ya Saruji 115,tofali 700 na tripu 5 ya mchanga.
Diwani wa kata ya Mabatini,Deus Lucas alisistiza wakazi wa kata ya mabatini wajitoa sana katika kuhakikisha wanajitoa kwa wingi ili kuleta maendeleo katika kata yao.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment