Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Wednesday 7 March 2018

WANANCHI LINDENI NA KUTUNZA VYANZO VYA MAJI

 Waziri wa Nishati Dkt. Merdad Kalemani akizungumza wakati wa Warsha ya Wadau wa  Mradi wa kuzalisha umeme Rufiji wa Megawati 2100 iliyofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mkoani Iringa.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamis Mwinyimvua akizungumza wakati wa Warsha ya Wadau wa  Mradi wa kuzalisha umeme Rufiji wa Megawati 2100 iliyofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mkoani Iringa.
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza wakati wa Warsha ya Wadau wa  Mradi wa kuzalisha umeme Rufiji wa Megawati 2100 iliyofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mkoani Iringa.
 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akizungumza wakati wa Warsha ya Wadau wa  Mradi wa kuzalisha umeme Rufiji wa Megawati 2100 iliyofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mkoani Iringa.
 Waziri wa Nishati dkt. Merdad Kalemani na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamis Mwinyimvua wakiteta jambo wakati wa Warsha ya Wadau wa  Mradi wa kuzalisha umeme Rufiji wa Megawati 2100 iliyofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mkoani Iringa.
Naibu wa Nishati, Subira Mgalu na Mkuu wa mkoa Iringa Amina Masenza wakiteta jambo wakati wa Warsha ya Wadau wa  Mradi wa kuzalisha umeme Rufiji wa Megawati 2100 iliyofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mkoani

Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani (kushoto) Naibu waziri wa Nishati (katikati) na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza (kulia) wakiwa nje ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Iringa.
washiki wa Warsha ya Wadau wa  Mradi wa kuzalisha umeme Rufiji wa Megawati 2100 iliyofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mkoani Iringa.

 Na Zuena Msuya , Iringa
Waziri wa Nishati Dkt.Kalemani amewataka Viongozi wa Serikali za Mitaa,Vijiji na wadau mbalimbali kuwaelimisha Wananchi juu ya umuhimu wa kutunza na kulinda vyanzo vya maji nchini ili yatumike kuzalisha umeme mwingi na pia katika matumizi bora ya Kilimo cha umwagiliaji.

Dkt.Kalemani alisema hayo wakati wa Warsha ya Wadau wa  Mradi wa kuzalisha umeme Rufiji wa Megawati 2100 inayofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mkoani Iringa.

Warsha hiyo ilishirikisha wadau mbalimbali wakiwemo Wakuu wa Wilaya, Wabunge, Viongozi wa Serikali za Mitaa na Vijiji ili kupata Elimu kuhusu faida na umuhimu wa kutunza vyanzo vya maji yanayoingiza maji yake katika bonde la Mto Rufiji patakapojengwa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa megawati 2,100 kwa kutumia maporomoko ya maji katika Bonde la  Mto Rufiji.

Katika warsha hiyo, Dkt.Kalemani alisema kuwa kutokana na kuwepo kwa Mradi mkubwa wa kuzalisha umeme kwa kutumia Maporomoko ya Maji katika bonde la Mto Rufiji, ni vyema Wananchi wakaelimishwa umuhimu wa kutunza maji kwa ajili ya Nishati ya umeme pamoja na matumizi mengine ikiwemo kilimo ili shughuli hizo zitekelezwe kwa pamoja pasipo kutokea athari yoyete.

Aliweka wazi kuwa mbali na Mradi huo kuzalisha umeme, pia eneo hilo litakuwa kivutio kikubwa cha utalii kwa kuwa lipo katika hifadhi ya Taifa ya mbuga ya wanyama ya Selou pamoja hivyo  kungizia Serikali mapato yatokanayo na utalii pamoja na biashara zitazokuwa zikiendeshwa katika eneo hilo.

Vilevile alisema kuwa Wizara zote zitashirikiana kutekeleza Mradi huo kwakuwa utekelezaji wake unahusisha Wizara mbalimbali zikiwemo Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Wizara ya Maliasili na Utalii, pamoja na Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano .

Alieleza zaidi kuwa hadi kufikia kwezi Julai  mwaka huu Mkandarasi atayetekeleza Mradi huo atakuwa amekwishapatikana na kuanza ujenzi wa mradi huo utakaokamilika kwa kipindi cha miaka 3, ambapo pamoja na mambo mengine kinachofanyika Sasa katika eneo la mradi huo ni ukamikishaji wa miundombinu ya Barabara, Reli , Maji pamoja na Umeme vitakavyotumiwa na mkandarasi wakati wa kutekeleza Mradi huo.

Nae Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, alieleza kuwa Mradi huo ni fursa kubwa ya ajira za muda mfupi na zile za muda mrefu kwa watanzania wenye taaluma husika na wale walio na uwezo na ujuzi.

Amewataka watanzania hasa Vijana kuchangamkia fursa hiyo katika kujiletea maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza aliahidi kutoa elimu kwa Wananchi wa Mkoa wa Iringa ambao sehemu kubwa ya mito yake hutiririsha maji katika Bonde la Mto Rufiji.

Aidha alisema kuwa ataendelea kuwaelimisha Wakazi wa Iringa kuweka njia Bora za kilimo cha umwagiliaji zitakazotumika katika kilimo badala ya ile iliyozoeleka ya kulima  Vinyungu katika vyanzo vya maji na Maeneo Oevu.

Kwa upande wao Wabunge wa Mkoa huo akiwepo Mbunge wa Mafinga mjini, Cosato Chumi  na mbunge wa kilolo Venance Mwamoto walisema kuwa watahakikisha Mradi huo unatekelezwa na hakutakuwa na changamoto zitakazoweza kuukwamisha Mradi huo kuanzia hatua za awali Hadi mwisho.

Walisema kwa kutumia nafasi zao watawashirikisha Wabunge wenzao kuhamasisha na kusimamia utekelezaji wa Mradi huo wenye manufaaa makubwa kwa Wananchi na Taifa kwa jumla.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment