Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Wednesday 31 January 2018

MLIOPOTEZA VYETI FUATENI UTARATIBU KUPATIA VYETI VINGINE

Na Katuma Masamba, Dodoma
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha amesema, mhitimu aliyepoteza cheti anapaswa kufuata taratibu zote ili aweze kupatiwa cheti kingine.

Amezitaja taratbu hizo kuwa ni pamoja na kutoa taarifa polisi kuhusu upotevu wa cheti na kupata hati ya upotevu, kutangaza gazetini kuhusu upotevu wa cheti  kwa lengo la kuutarifu umma ili kusaidia kupatacheti kilichopotea.

“Lengo la kutoa taarifa polisi ni ni kupata msaada wa kiuchunguzi ili kusaidia kukipata cheti kilichopotea,” amesema Nasha.

Akijibu swali la Mbungewa Mafinga Mjini, Cosato Chumi aliyetaka kujua taratibu zinazotumika kwa mtu aliyepoteza cheti cha taaluma, Nasha amesema endapo cheti kilichopotea hakikupatikana hata baada ya kutangazwa, mhusika atalazimika kujaza fomu ya omb la cheti mbada;a au uthibitisho wa matokeo na kuiwasilisha Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) na kwenye tovuti  ya baraza hilo.

Amesema NECTA pia hufanya uchunguzi wa uhalali wa umiliki wa ccheti husika na kutoa huduma stahiki. Wahitimu waliofanya mitihani kuanzia mwaka 2008 ambao vyeti vina picha hupatiwa vyeti mbadala  huku waliofanya mitihani kabla ya mwaka huo hupatiwa uthibitishowa matokeo.

Nasha pia amebainisha kuwa cheti mbadala kinachotolewa ni halisi, lakini huongezwa maandishi yanayosomeka ‘DUPLICATE’ kuonesha kuwa cheti hicho kimetolewa mara ya pili.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment