Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 1 December 2017

TLB KWIMBA WAHIMIZA UPANDAJI MITI

Mratibu wa chama cha wasioona wilayani Kwimba Isack Manumbu akipanda mti katika zahanati ya Malemve katika kata ya Igongwa.
****************
Na Alexander Sanga,Kwimba
Uongozi wa Chama cha wasioona wilayani hapa(TLB_Kwimba) imewahimiza wadau mbali mbali kuhakikisha wanapanda miti katika maeneo yao ili kuepeka kujitokeza kwa tatizo la ukame.

Akizungumza katika zoezi la upandaji miti katika Zahanati ya Malemve kichopo kata ya Igongwa,Mratibu wa chama hicho Isack Manumbu alisema wameanza kupanda miti 300 katika zahanati hiyo ila bado chama chao kina mikakati ya kupanda miti zaidi wilayani hapo.

Kwa upande wake afisa mali asili wilayani Kwimba Joseph Swai alisema hali ya miti wilayani kwake sio nzuri kwakuwa kuna idadi kubwa ya ukataji miti kutoka kwa wakazi wa wilayani hapo.

Swai alisema kwa mwaka huo Halmashauri yao ina mikakati ya kupanda miti milioni 1,500,000/- katika kata zote 30 za wilayani hapo.

Joseph aliiomba pia serikali ipunguze bei ya gesi ili wananchi waache kukata miti kwajili ya kupata kuni.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment