Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Saturday 30 December 2017

MKUCHIKA AWASILISHA FOMU YA TAMKO LA RASILIMALI NA MADENI-MTWARA

Waziri wa NchiOfisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Capt Mstafu George Mkuchika Akikabidhi Fomu za tamko la Rasilimali na Madeni kwa Katibu Msaidi wa Tume ya serkretarieti ya Maadili ya Utumishi wa Umma Kanda ya Kusini Mayina Henjewele.
Waziri wa NchiOfisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Capt Mstaafu George Mkuchika akionesha Fomu ya tamko Mara baada ya kukabidhi Fomu zake na Kuhakikiwa.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Tume ya Sekretarieti ya Maadili ya Utumishi wa Uma Kanda ya Kusini Mayina Henjewele akisoma Taarifa kuhusiana na Viongozi waliokwisha Wasilisha Fomu za tamko la Rasilimali na Madeni katika Mikoa ya Ruvuma,Lindi na Mtwara.
*****************
Waziri wa NchiOfisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Capt Mstaafu, George Mkuchika  amewataka Wabunge,madiwani na Viongozi wa Umma wanaojihusisha na Biashara na Halmashauri kuacha mara moja kutokana na Kwenda kinyume na sheria ya viongozi na watumishi wa umma.

Mkuchika ameyasema hayo wakati akirejesha fomu za tamko la Rasilimali na Madeni katika Ofisi ya sekretarieti ya maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kusini Iliyopo Mkoani Mtwara.

Mpaka Kufikia Sasa Jumla ya Viongozi 794 ndio wamerejesha fomu hizo za tamko la Rasilimali na Madeni kati ya Viongozi 1246 ambao wanatakiwa kuwasilisha kwa kanda hiyo.

Aidha Ofisi hiyo imetenga Siku ya Jumapili, Desemba 31,2017  kuanzia Mchana mpaka Jioni Kupokea fomu kwa Viongozi ambao hawajawasilisha.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment