Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 1 December 2017

SERIKALI KUJENGA VITUO VYA AFYA 172

Na Alexander Sanga, DodomaWaziri wa Tawala za mikoa na serikali za mitaa Seleman Jafo amesema serikali inaendelea na ujenzi wa vituo vya Afya 172 ambapo vinatarajia kukamilika tarehe 30 Desemba mwaka huu.

Akizungumza katika kipindi cha Tujadiliane kilichoandaliwa na umoja wa vilabu vya vyama vya waandishi wa habari nchini(UTPC),Jafo alisema serikali kila kituo tumepeleka milioni 500.

"Hii ni kwa mara ya katika historia ya nchi hii kujenga vituo vya Afya 172 ndani ya miezi minne na kila kituo tumepeleka milioni 500 tunajenga kliniki ya watoto,maabara,Mochuwari na Theatre" Jafo alisema.

Waziri Jafo alisema kila bado kuna tatizo kubwa sana la Afya na kwa sasa sera ya serikali ni kuhakikisha kila kijiji kiwe na kituo cha afya.

Akielezea kuhusiana na suala la sawa,Jafo alisema serikali imetenga bilioni 269 za bajeti ya sawa kwa mwaka huu wa fedha 2017/18.

Suleiman aliwapongeza wabunge wenzake kwa kusaidia kwenye ujenzi wa zahanati katika maeneo yao.

Jafo alisema suala la vyeti feki na watumishi hewa nilikuwa changamoto kubwa sana katika sekta ya afya lakini serikali mpaka sasa imepambana na kufanikiwa kuajiri watalamu wa afya 2058 katika maeneo mbali mbali nchini.

Katika sekta ya Elimu waziri Jafo alisema serikali itahakiksha inaajiri walimu 2700 kwa mwaka kwa shule za msingi na sekondari mpaka mwishoni mwa Disemba na pia alisema wanatarajia kuajiri walimu 11000 ambapo walimu wa shule ya msingi watakuwa 7000 na sekondari 4000.

Jafo alisema suala la mimba mashuleni bado ni kero kubwa sana na serikali mwezi Agosti ilitenga bilioni 16 kwajili ya ujenzi mabweni kwa shule 63 za sekondari nchini.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment