Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Monday 13 November 2017

ELIZABETH MICHAEL AU LULU NINANI?

MUIGIZAJI na Muongozaji Filamu, Elizabeth Michael (Lulu) ,22, leo amehukumuiwa kifungo cha Miaka Miwili gerezani  baada ya Mahaka Kuu Tanzania, kumtia hatiani kwa kosa la kumuua Bila kukusudia. Anaandika Mroki Mroki wa Daily News Digital. 

Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam, imemuhukumu msanii maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael Kimemeta kutumikia kifungo cha miaka miwili gerezani baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya bila kukusudia ya msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba.

Hukumu hiyo imesomwa na Jaji Sam Rumanyika ambaye amesema, ameridhika na ushahidi wa mashahidi wanne wa upande wa mashitaka na wazee wa baraza waliotoa maoni yao kuwa kweli mshtakiwa Lulu aliuwa bila ya kukusudia.

Alisema  Aprili 12, 2012 ndio ilikuwa mara ya kwanza kwa Lulu kufikishwa Mahakamani ambapo alifikishwa katika mahakama ya mkoa wa Dar es Salaam, ambayo ni Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kujibu tuhuma za mauaji ya marehemu Kanumba.

Lakini baadae baada ya kusota rumande kwa takribani miezi kumi, Lulu alibadilishiwa mashitaka na kushitakiwa kwa mauaji ya bila kukusudia, shtaka lililomuwezesha kuwa nje kwa dhamana hadi leo.

Tukio hilo lilitokea mnamo Aprili 6, 2012 huko Sinza Vatcan jijini Dar es Salaam wakati ikielezwa kuwa wasanii hao wawili wakiwa ni marafiki wakaribu.

LAKINI ELIZABETH AU LULU NINANI?

Diana Elizabeth Michael Kimemeta kama alivyotambulika na wazazi wake, Michel Kimemeta na mama Lucrecia Kalugira alizaliwa Aprili 16,1995. Baadae alianza elimu ya Msingi katika shule ya Remnant baadaadae katika sekondari za Perfect Vision na St Mary’s za jijini Dar es Salaam na kujiunga na elimu ya juu pale alipojiunga na Chuo cha utumishi wa Umma kuchukua Diploma ya Meneja Rasilimali watu.

Lulu alianza kuonesha kipaji chake cha ugizaji akiwa bado mtoto na hapa ni akiwa na umri wa miaka mitano tu, pale Mwigizaji Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ alipomchukua na kujiunga nae katika Kundi la Sanaa la Kaole.

Baada ya kujiunga na Kaole Lulu alianza kushiriki na kuonekana katika michezo mbalimbali ya kuigiza ya kundi hilo iliyokuwa iukirushwa na ITV na miongoni mwa michezo hiyo ni pamoja na  Zizimo, Dira, BaragumuGharikaTaswira, Tufani, Tetemo, Jahazi, Sarafu na Demokrasia.

Mwaka 2005 Lulu alianza kuingia katika filamu ambapo alianza kutoa filamu yake ya kwanza iliyojulikana kama Misukosuko. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

Pia aliwahi kushiriki katika michezo ya kuigiza ya Redioni kama ule wa Wahapahapa lioshiriki mwaka 2009, pia alichez mchezo wa Mainda ambao ulilenga kutoa elimu ya umuhimu wa mawasiliano baina ya mzazi na mtoto katika kulinda vijana wakati wa makuzi yao.

Lulu pi ameshiriki na kuonekan katika filamu mbalimbali na majririda maalum zaidi ya 30. Mwezi Agosti mwaka 2013 alizindua filamu yake aliyoipa jina la Foolish Age, ambayo mbali na kushirtiki kuicheza lakini alikuwa pia kama mtaryarishaji wa Filamu hiyo.

Filamu hiyo iliyozinduliwa Mlimani City jijini Dar es Salaam ilichaguliwa kuwa miongoni mwa filamu zilizooneshwa katikia Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar (ZIFF) ya mwaka 2014.

Filamu ya Foolish Age  ilichaguliwa tena katika Tuzo za watu 2014 ambapo ilishinda tuzo ya Filamu iliyopendwa huku yeye mwenyewe akishinda tuzo ya Mwigizaji aliyependwa katika Filamu hiyo.

 Mwaka 2015 aliachia filamu yake ya pili kama Mtayarishaji, ambayo ilienda kwa jina la Mapenzi Ya Mungu . Tuzo hiyo kama ilivyokuwa kwa ile ya Foolish Age nayo iliyoneshwa katika Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar (ZIFF) 2015 na kujishindia Tuzo ya 2016 Africa Magic Viewers Choice Awards kama Filamu Bora ya Afrika Mashariki.

Mwaka uliofuata 2016 alitoa filamu mpya ya tatu aliyoipa jina la Ni Noma ambayo ilikuwa ikiuzwa kupitia mitandao katika App malum ya ProinBox

Ubalozi

Mwaka 2013 alichaguliwa kuwa Balozi wa Tamasha la Filamu Dar es Salaam (DFF) ambapo pia filamu yake ya Foolish Age ilioneshwa katika tamasha hilo.

Mnamo mwaka 2014 Lulu aliingia mkataba na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel kuwa Muongozaji wa kipindi  Airtel Yatosha TV Show.

Mwaka 2015, Lulu alisaini mkataba na wa kuwa Balozi wa Paisha Tanzania ambapo alikuwa Balozi wa App ya Paisha ambayo ilikuwa ikijihusisha na biashara mtandaoni.

Aliendelea zaidi kung’ara  na mwaka  2016, alitangaza  na kampuni ya Hengan Baby Products & Sanitary Co. Ltd. (Tanzania) kuwa Balozi wa bidhaa yake ya  taulo za akina mama za Freestyle.

Mwezi Oktoba Mwaka huu, Azam Media Tanzania kupitia Chaneli yake ya Sinema zetu, ilimtangaza Lulu kuwa Balozi Maalum wa Tamasha la Kimataifa la Filamu la Sinema Zetu (SZIFF).



Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment