Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday, 24 August 2017

TANZANIA YAPOKEA MUALIKO WA KUJIUNGA NA UMOJA WA HIYARI WA MABUNGE YA AFRIKA (APU).

Spika wa Bunge la Tanzania; Job Ndugai (kulia) akipokea mwaliko maalum wa kujiunga na Umoja wa hiari wa Mabunge ya Afrika (APU) kutoka kwa Mwenyekiti wa umoja huo na Spika wa Bunge la Guinea Bisau; Cipriano Cassama katika ofisi ndogo za Bunge; Dar es Salaam jana. (Picha na Mroki Mroki).
 Spika Ndugai akiwa na Mgeni wake Spika wa Bunge la Guinea Bisau, Cassama.
BUNGE  la Tanzania limepokea mwaliko kutoka kwa Spika wa Bunge la Guinea Bissau, Cipriano Cassama wa kujiunga  kwenye Umoja wa hiari wa Mabunge ya Afrika (APU) ambao wanaongea lugha nne na kuwapatia vitendea kazi, kanuni na taratibu za kujiunga.

Mbali na Cassama ujumbe huo pia uliambatana na Katibu Mkuu wa APU, NZI Koffi na wawakilishi wengine kutoka nchi za Ghana na Senegal.

Ndugai alisema ‘’bunge hilo linatumia lugha za Kifaransa, Kireno, Kiarabu na Kiingereza ambapo ni tofauti na bunge la Jumuiya ya Madola tulilojiunga nalo ambalo linatumia lugha moja pekee ya Kiingereza.’’

Alisema kuwa taratibu wa kujiunga na umoja huo utafanyika na kwamba watajibu mualiko huo mapema iwezekanavyo.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment