Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 17 February 2017

HALMASHAURI NA MIKOA MITANO YA KANDA YA ZIWA KUZINDUA TOVUTI ZAKE ZA HALMASHAURI NA MIKOA WIKI IJAYO



Mtafiti Mwandamizi  Mshiriki kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta (PS3), Dk.Fenohasina Rakotondrazaka, akitoa mada kwa Maofisa Habari na Tehama kutoka Halmashauri na Mikoa ya Kanda ya Ziwa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Kagera na Simiyu wanaoshiriki mafunzo elekezi ya uwekaji wa taarifa katika tovuti yaliyoandaliwa na PS3 na kufanyika jijini Mwanza.

Na Mroki Mrok, TSN Digital Mwanza

KATIKA kuhakikisha Serikali inaboresha usimamizi wan a ushirikishwaji wa wananchi katika Nyanja ya habari na mawasiliano kwa umma, Maofisa habari na Tehama kutoka Sekreatarieti za mikoa mitano na mamlaka za Serikali za mitaa 37 kutoka katika kanda ya Ziwa wapo jijini Mwanza kwaajili ya mafunzo maalum ya uendeshaji tovuti zao.



Takribani juma moja maofisa hao watapatiwa mbinu mbalimbali za kuendesha tovuti zao ambazo mapema wiki ijayo zinataraji kuzinduliwa baada ya mafunzo kwa maofisa hao kukamilika.



Mradi huo unaendeshwa ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)  ni mradi wa miaka mitano ambao unatekelezwa na unafanya kazi na Serikali Kuu pamoja na Halmashauri 93 katika mikoa 13 ya Tanzania bara.



PS3 inaimarisha mifumo ya sekta za umma yakiwemo masuala ya utawala bora, rasilimali watu, fedha, utoaji wa taarifa, na tafiti tendaji.



Ushirkiano huu wa PS3 katika ngazi ya Serikali kuu na Halmashauri, una nia ya kukuza utoaji, ubora, na matumizi ya huduma za umma, hususani kwa jamii ambazo hazijanufaika vya kutosha.



Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Wakala wa Serikali Mtandao (eGA), Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Shirika la Kimarekani la Misaada ya Kimaendeleo (USAID) waliunda mfumo ambao utafanya kazi ya kuhuisha mfumo kwa kushirikisha taarifa ambazo zitajenga ufanisi, uwazi na uaminifu wa umma.

Maofisa Habari na Tehama kutoka Halmashauri na Mikoa ya Kanda ya Ziwa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Kagera na Simiyu wakishiriki katika  mafunzo elekezi ya uwekaji wa taarifa katika tovuti yaliyoandaliwa na Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) na kufanyika jijini Mwanza.

Maofisa Habari na Tehama kutoka Halmashauri na Mikoa ya Kanda ya Ziwa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Kagera na Simiyu wakishiriki katika  mafunzo elekezi ya uwekaji wa taarifa katika tovuti yaliyoandaliwa na Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) na kufanyika jijini Mwanza.
Mofisa Habari na Tehama wakiwasilisha tovuti zao.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment