Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 28 July 2017

WANAHABARI WAASWA KUTOANDIKA HABARI ZITAKAZOATHIRI UTALII NCHINI


Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dk. Hassan Abbas akiwasilisha mada kuhusu majukumu ya vyombo vya habari katika sekta ya utalii kwa wahariri na wanahabari waandamizi katika mkutano wa sita ulioandaliwa na Hifadhi za Taifa (TANAPA) mkoani Tanga.
VYOMBO vya habari nchini havipaswi kuandika mambo ambayo yanaweza kuathiri utalii wa Tanzania na badalayake vinapaswa kuwa chachu ya kukuza na kuutangaza utalii. Anaandika Katuma Masamba-Tanga.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dk. Hassan Abbas, amesema wanahabari wanapaswa kuhakikisha wanaandika mambo ambayo yataweza kuwavutia watalii kuja nchini na kutembelea vivutio mbalimbali hatua ambayo itasaidia kukuza pato la taifa.

Akizungumza wakati wa kuwasilisha mada ya wajibu wa vyombo vya habari katika sekta ya utalii kwenye mkutano wa wahariri na wanahabari waandamizi wa kujadili sekta ya utalii nchini unaoendelea jijini Tanga.

"Tunaweza kutumia vyombo vyetu vya habari kuandika vizuri habari za utalii na sekta nzima ya utalii, kwa mfano Kenya huwezi ukakuta wanaandika jambo ambalo wanaona linaweza kuiathiri nchi yao," amesema Dk Abbas.

Waandishi mbalimbali wa habari nchini wakisikilza mada wakati wa mkutano wa Hifadhi za Taifa, Wahariri na Waandishi wa habari waandamizi nchini unaofanyika jijini Tanga.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment