Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Saturday 27 May 2017

SIMBA MABINGWA WAPYA WA KOMBE LA FA TANZANIA BARA

TIMU ya Soka ya Simba ya Jijini Dar es Salaam leo imetazwa rasmi kuwa Mabingwa wa Michuano ya Kombe la Shirikisho Tanzania Bara (FA) baada ya kuilaza Mbao FC ya Jiji Mwanza kwa mabao 2-1 katika mtanange wa vuta ni kuvute uliochezwa kwa dika 120 katika dimba la Jamhuri Mjini Dodoma leo. Anaandika Mroki Mroki-Dodoma.

Simba na Mbao zilicheza mbele ya mshabiki lukuki kutoka mji wa Dodoma na mikoa jirani wakiongozwa na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, ambapo pia mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe.


Kufuatia ushindi huo sasa Simba itaiwakilisha nchi katika Michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Simba imekuwa timu ya pili kutwa kombe hilo la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) tangu kuanzishwa ambapo watani zao Yanga ndio walikuwa wakwanza kutwaa kombe hilo.

Aliyewainua viti maelfu ya mashabiki wa Simba alikuwa ni mchezaji wa kimataifa wa Simba, mzaliwa wa Ivory Coast, Frederick Blagnon baada ya kuipatia timu yake bao la kuongoza kunako dakika ya 95 na kuamsha matumaini ya wakongwe hao wa Mtaa wa Msimbazi ya kutwaa ubingwa wa FA.

Dakika ya 109 ya mchezo huo mchezaji wa Mbao FC, Robert Ndaki alizima furaha za Simba uwanja wa Jamhuri na viunga vya Mji wa Dodoma ambao tayari walianza kushangilia ubingwa kwa kuifungia timu yake bao safi kufuatia makosa ya walinzi wa Simba na kupiga majalo iliyo mpita mlinda mlango wa Simba.

Dakika ya 119 palitokea piganikupige katika lango la yanga na katika harakati za kuokoa mpira mchezaji wa Mbao aliunawa mpira na mwamuzi wa Ahmed Kikumbo kutoka Dodoma kuamuru mwaju wa penati upige ambapo almanusra mwamuzi aambulie kichapo.

Chiza Kichuya alipiga mkwaju wa penati kunako dakika ya 120 ishirini ambapo bao hilo lilidumu hadi kipenga cha mwisho Simba 2 na mbao 1.

Vikosi vya timu zote mbili vilivyoshuka dimbani hii leo ni
MBAO FC: Benedict Haule, Asante Kwasi, Yussuf Ndikumana, David Mwasa, Salmin Hozza, Boniface Maganga, George Sangija/Dickson Ambundo dk59/Rajesh Kotecha dk104, Jamal Mwambeleko, Pius Buswita, Habib Hajji/Robert Ndaki dk104 na Ibrahim Njohole: KOCHA: Etienne Ndayiragile

SIMBA SC: Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tahabalala’/Abdi Banda dk51, James Kotei, Juuko Murshid, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Muzamil Yassin, Laudit Mavugo, Said Ndemla/Frederick Blagnon dk80 na Juma Luizio/Ibrahim Hajib dk60. KOCHA: Joseph Omong

WAAMUZI: Ahmed Kikumbo alisaidiwa na Mohamed Mkono na Omary Juma lakini Msimamizi wa Mchezo alikuwa Florentina Zablon. 


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment