Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday 18 May 2017

POLISI YATOA UFAFANUZI KUHUSU MATUMIZI YA FOMU NAMBA TATU YA POLISI (PF3).



               Msemaji wa Jeshi la Polisi ACP-Advera Bulimba
 
JESHI  la Polisi nchini li limetoa ufafanuzi kuwa, Fomu ya Polisi namba 3 ijulikanayo kama PF.3 hutolewa  kwa mtu baada ya Polisi kupata taarifa kutoka kwa mlalamikaji au muathirika  kwa matukio yenye madhara mwilini, ajali au  matukio yenye kuleta mashaka kuhusu vyanzo vyake kama vile kipigo, kujeruhi, ubakaji, kulawiti,  kunywa sumu na mengineyo.

Msemaji wa Jeshi la Polisi, ACP, Advera Bulimba katika katika taarifa yake kwa umma amesema kuwamatumizi ya PF3 bado ya naendelea na ni yalazima kwa mujibu wa sheria hivyo inapaswa kutumika kwa kila tukio.

"Ieleweke wazi kwamba matumizi ya PF3 ni ya lazima na yanaendelea kama kawaida  kwa mujibu wa sheria, fomu hiyo inapaswa kutumika kwa kila tukio la aina tajwa hapo juu ili muathirika  aweze kupata matibabu katika vituo vya Afya na hatua za kiupelelezi  kwa Jeshi la Polisi ziweze kuendelea,"alisema ACP Bulimba.  

ACP Bulimba amesema Katika mazingira mengine hali ya muathirika inaweza kuwa mbaya, hivyo,  huduma za kuokoa maisha (huduma ya kwanza) zinaweza kuendelea kutolewa wakati watoa  huduma ya afya wakiijulisha Polisi  ili kuharakisha upatikanaji wa PF 3.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment