Home
About Us
Siasa
Uchumi
Biashara
Michezo
Burudani
Wasiliana Nasi
Have you got a good story?
Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.
Have you got a good story?
Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.
Saturday 6 May 2017
NEC YATOA UFAFANUZI UTARATIBU WA KUMPATA MBUNGE NA DIWANI VITI MAALUM
Saturday, May 06, 2017
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeeleza kuwa nafasi za Wabunge wa Viti Maalum wanaoteuliwa zipo kwa mujibu wa Sheria na zimeainishwa katika Ibara ya 78 (1) na (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.
Akitoa ufafanuzi huo leo jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani amesema kuwa Ibara ya 78 (1) na (4) ya Katiba inaeleza utaratibu mzima wa kuwapata Wabunge wanawake wa Viti maalum.
Amesema kila Chama cha Siasa kinachoshiriki katika Uchaguzi Mkuu na kupata angalau asilimia 5 ya Kura zote halali za wabunge kitapata Wabunge wa Viti Maalum kulingana na Kura ambazo chama husika kimepata.
Amefafanua kuwa Chama kinachopata asilimia 5 ya Kura zote halali za Wabunge katika Uchaguzi Mkuu kinatakiwa kuwasilisha orodha ya wanachama wanaopendekezwa kuwa wagombea wa Viti Maalum ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Aidha, ameeleza kuwa endapo inatokea nafasi wazi ya Mbunge wa Viti Maalum katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokana na sababu mbalimbali, Spika wa Bunge humtaarifu Mwenyekiti wa Tume juu ya uwepo wa nafasi hiyo kwa mujibu wa kifungu cha 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343.
Amesema kuwa Mwenyekiti wa Tume hukiandikia barua chama husika kukitaarifu juu ya uwepo wa nafasi wazi ya viti maalum ili kiweze kuwasilisha pendekezo la jina katika orodha kiliyowasilishwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi mwaka 2015, ikiambatanishwa na Fomu namba 8 D ya kuomba jina lililopendekezwa liteuliwe na Tume katika nafasi ya Ubunge kulingana na sifa zilizoainishwa kwa mujibu wa Sheria.
Saturday, May 06, 2017
Copyright: Dailynews Blog
Mtumie Rafiki Yako
Maoni: 0
Email This
BlogThis!
Share to Twitter
Share to Facebook
Newer Post
Older Post
Home
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
Tags
Kumbu Kumbu
KARIA AMTEUA NYAMLANI, MGOYI KUONGOZA KAMATI ZA TFF PIA WAMO WAANDISHI WAWILI WA TSN
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Wallace Karia amewateua Makamu wa Rais wa zamani wa TFF, Athuman Nyamlani na Ahmed Mgoyi ...
UTAFITI: WANANCHI WENGI WAMEKUMBWA NA NJAA KATIKA KIPINDI CHA MIEZI MITATU ILIYOPITA
IDADI kubwa ya wahojiwa wa Sauti za Wananchi (asilimia 78) wameripoti uhaba wa chakula katika maeneo wanayoishi. Hali ni mbaya zaidi k...
MAJALIWA ATEMBELEA KIWANDA CHA CHAI CHA LUPEMBE NA KUZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa kiwanda cha chai cha Lupembe, Mussa Kefa (kushoto kwake)...
KAJEMBE; MZARAMO ALIYEUTEKA MJI WA MOSHI KWA BIASHARA YA KUKAANGA MIHOGO
WAANDISHI wa Habari ni watu wa kuzunbuka sana nchini na Duniani kwa ujumla katika harakati za utafutaji habari za kuhabarisha jamii juu ...
MTOTO MICHAEL KADUNGALA AOMBA MSAADA WA MATIBABU
MTOTO Michael Kadungala (15) mwenye ulemavu wa kutoona amemwomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk. John Magufuli amsaidie awe...
AMINA MOLLEL: WAZAZI MSIWAFICHE WATOTO WENYE ULEMAVU NDANI
Mbunge wa viti maalumu CCM Amina Mollel akiwa anacheza ngoma ya kimasai pamoja na baadhi ya wamasai waliojitokeza katika sherehe za ku...
MZEE NDESAMBURO KUAGWA UWANJA WA MASHUJAA MOSHI KABLA YA MAZIKO JUNI 6 MWAKA HUU
Kikao cha Wanafamilia,Viongozi wa siasa na Viongozi wa Dini kikifanyika nyumbani kwa marehemu Ndesamburo kwa ajili ya maandalizi ya mazis...
YALIYOJIRI BUNGENI MJINI DODOMA LEO APRILI 10,2017
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Tulia Ackson akiongoza kikao cha nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 lina...
RAIS MAGUFULI ATAKA TAKUKURU KUCHUNGUZA UHALALI WA MKATABA WA MANISPAA NA WAKALA WA MAEGESHO MOSHI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na viongozi wa dini wa mkoa wa Kilimanjaro baada ya kupat...
WIZARA YA MALIASILI KWA KUSHIRIKIANA NA SPANEST KUTOA MAFUNZO YA HUDUMA KATIKA SEKTA YA UTALII NA UKARIMU KWA MIKOA YA MBEYA, NJOMBE NA IRINGA
Labels
BURUDANI
MICHEZO
SIASA
Kumbu Kumbu
January
(86)
February
(95)
March
(131)
April
(117)
May
(113)
June
(127)
July
(81)
August
(69)
September
(46)
October
(55)
November
(21)
December
(47)
January
(66)
February
(32)
March
(41)
April
(40)
May
(27)
June
(9)
October
(1)
BLOG MBALI MBALI
Father Kidevu
SERIKALI INAENDELEA KUWAHUDUMIA WAATHIRIKA WA KIMBUNGA IDAYA - MAJALIWA
MICHUZI BLOG
Rais Samia azindua Kiwanda cha kuunganisha Malori na Matipa cha Saturn Corporation Limited Kigamboni Jijini Dar es Salaam
HABARI LEO
Arusha on spotlight
OFA YA MATANGAZO
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment