Home
About Us
Siasa
Uchumi
Biashara
Michezo
Burudani
Wasiliana Nasi
Have you got a good story?
Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.
Have you got a good story?
Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.
Saturday, 6 May 2017
NEC YATOA UFAFANUZI UTARATIBU WA KUMPATA MBUNGE NA DIWANI VITI MAALUM
Saturday, May 06, 2017
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeeleza kuwa nafasi za Wabunge wa Viti Maalum wanaoteuliwa zipo kwa mujibu wa Sheria na zimeainishwa katika Ibara ya 78 (1) na (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.
Akitoa ufafanuzi huo leo jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani amesema kuwa Ibara ya 78 (1) na (4) ya Katiba inaeleza utaratibu mzima wa kuwapata Wabunge wanawake wa Viti maalum.
Amesema kila Chama cha Siasa kinachoshiriki katika Uchaguzi Mkuu na kupata angalau asilimia 5 ya Kura zote halali za wabunge kitapata Wabunge wa Viti Maalum kulingana na Kura ambazo chama husika kimepata.
Amefafanua kuwa Chama kinachopata asilimia 5 ya Kura zote halali za Wabunge katika Uchaguzi Mkuu kinatakiwa kuwasilisha orodha ya wanachama wanaopendekezwa kuwa wagombea wa Viti Maalum ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Aidha, ameeleza kuwa endapo inatokea nafasi wazi ya Mbunge wa Viti Maalum katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokana na sababu mbalimbali, Spika wa Bunge humtaarifu Mwenyekiti wa Tume juu ya uwepo wa nafasi hiyo kwa mujibu wa kifungu cha 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343.
Amesema kuwa Mwenyekiti wa Tume hukiandikia barua chama husika kukitaarifu juu ya uwepo wa nafasi wazi ya viti maalum ili kiweze kuwasilisha pendekezo la jina katika orodha kiliyowasilishwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi mwaka 2015, ikiambatanishwa na Fomu namba 8 D ya kuomba jina lililopendekezwa liteuliwe na Tume katika nafasi ya Ubunge kulingana na sifa zilizoainishwa kwa mujibu wa Sheria.
Saturday, May 06, 2017
Copyright: Dailynews Blog
Mtumie Rafiki Yako
Maoni: 0
Email This
BlogThis!
Share to X
Share to Facebook
Newer Post
Older Post
Home
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
Tags
Kumbu Kumbu
RAIS MAGUFULI ATAKA TAKUKURU KUCHUNGUZA UHALALI WA MKATABA WA MANISPAA NA WAKALA WA MAEGESHO MOSHI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na viongozi wa dini wa mkoa wa Kilimanjaro baada ya kupat...
MASALIA YA MIJUSI (DINOSOUR) MIKUBWA KUTORUDISHWA NCHINI
Na Octavian Kimario-WHUSM Dodoma. Wazo la kuwarudisha nchini Dinosaria halina tija kutokana na ugumu wa Kiteknolojia na gharama ikili...
RAIS MAGUFULI AMTEUA PROF KITILA MKUMBO KUWA KATIBU MKUU WIZARA YA MAJI NA UMWAGILIAJI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 04 Aprili, 2017 amefanya mabadiliko madogo katika ...
ASKOFU DK. MALASUSA AZINDUA TAWI LA MAENDELEO BANK KARIAKOO
Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa akiweka fedha mara baada y...
SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI KUFANIKISHA TANZANIA YA VIWANDA.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema serikali inathamini mchango wa sekta binafsi na itaendelea kushirikiana nayo katik...
KUANZA KUTUMIKA SHERIA YA HUDUMA ZA HABARI, 2016 NA KANUNI ZAKE, 2017
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa Habari Mjini Dodoma leo kuhusiana kuanza kutumik...
RAIS MAGUFULI AAHIDI KUFANYA ANNUAL INCREMENT YA MSHAHARA NA PROMOSHENI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wafanyakazi katika kilele cha Sikukuu ya Wafanya...
KUPIGA CHAPA MIFUGO NCHI NZIMA MWISHO JANUARI 31,2018
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Maria Mashingo akipiga chapa ng’ombe katika Kijiji cha Igalula Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Ka...
MBUNGE WA CHALINZE AKANUSHA YALIYOANDIKWA KATIKA MTANMDAO WAKE WA INSTAGRAM
CCM Z'BAR YATOA POLE KWA WANANCHI WALIOPATA ATHARI ZINAZOTOKANA NA MVUA
Picha mbalimbali zikionyesha athari za Mvua kisiwani Zanzibar. CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kinatowa pole kwa wananchi ...
Labels
BURUDANI
MICHEZO
SIASA
Kumbu Kumbu
January
(86)
February
(95)
March
(131)
April
(117)
May
(113)
June
(127)
July
(81)
August
(69)
September
(46)
October
(55)
November
(21)
December
(47)
January
(66)
February
(32)
March
(41)
April
(40)
May
(27)
June
(9)
October
(1)
BLOG MBALI MBALI
MICHUZI BLOG
MAANDALIZI YA KUPOKEA MWENGE WA UHURU YAKAMILIKA ARUSHA, ALI KIBA NA JUMA NATURE KUPAMBA MKESHA
Father Kidevu
TUENDELEE 'KUKIBIDHAISHA KISWAHILI' KUFANIKISHA UKUZAJI UCHUMI
HABARI LEO
Arusha on spotlight
OFA YA MATANGAZO
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment