Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 26 May 2017

MAONESHO YA VYUO VIKUU VYA INDIA KUFANYIKA KESHO

MAONESHO ya Vyuo Vikuu vya nchini India yanatarajiwa kufanyika kesho huku yakitarajiwa kutoa fursa kwa wanafunzi wa Kitanzania kuvifahamu vyuo vilivyopo nchini humo na ubora wa taaluma zake.

Maonesho hayo ambayo yameandaliwa na Global Education Link (GEL) kwa kushirikiana na Ubalozi wa India nchini yatafanyika kesho katika ubalozi huo uliopo jirani na Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC).

Akizungumzia maonesho hayo, Mkurugenzi wa Global Education Link, Abdulmalik Mollel amesema, wanafunzi wa kitanzania wamekuwa wakikumbana na changamoto kubwa ya kudsoma katika vyuo ambavyo havina ifa.

“Unakuta mwanafunzi anapewa taarifa ambazo si sahihi hata katika vyuo anachokwenda, na ndio sababu tumeamua kuandaa maonesho hayo ili kubaini vyuo sahihi,” alisema.
Amesema wanafunzo wengi wamejikuta wakisoma katika vyuo ambavyo havina hadhi sawa na ile waliyotegemea, hatua inayowawia vigumu katika kutambulika na Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU).

Kwa upande wake Balozi wa India nchini, Sandeep Arya amesema maonesho hayo yatafanyika Kesho na keshokutwa katika ubalozi wa India na kwamba lengo kubwa ni kuwaunganisha wanafunzi wa kitanzania wanaolenga kusoma katika nchi hiyo na vyuo vyenye ubora.

Arya amesema maonesho hayo yatashirikisha taasisi 20 za vyuo vikuu ambazo zinazotoa fani tofauti katika ngazi zote za elimu ya juu.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment