Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 16 January 2018

RAIS DKT MAGUFULI APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO TOKA KWA MABALOZI SITA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea baada ya kupokea hati ya utambulisho toka kwa balozi mpya wa Nigeria nchini, Sahabu Isah Gada Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari 16, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho toka kwa balozi mpya wa Poland nchini,  Krysztof Buzalski Ikulu jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea baada ya kupokea hati ya utambulisho toka kwa balozi mpya wa Uturuki nchini,  Ali Davutoglu Ikulu jijini Dar es salaam leo Alhamisi 16, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea baada ya kupokea hati ya utambulisho toka kwa balozi mpya wa Ufaransa mchini,  Frederic Clavier Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari 16, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho toka kwa balozi mpya wa Israel hap nchini, Noah Gal Gendler Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari 16, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho toka kwa balozi mpya wa Australia nchini,  Alison Chartres Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari 16, 2018.
*****************
RAIS Dkt. John Magufuli leo Januari 16, 2018 amepokea hati za utambulisho za Mabalozi 6 walioteuliwa kuziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Mabalozi waliowasilisha hati zao za utambulisho ni Balozi wa Nigeria hapa nchini, Sahabu Isah Gada, Balozi wa Poland hapa nchini , Krzysztof Buzalski, Balozi wa Uturuki hapa nchini, Ali Davutoglu, Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Frédéric Clavier, Balozi wa Israel hapa nchini, Noah Gal Gendler na Balozi wa Australia hapa nchini, Alison Chartres.

Akizungumza na Mabalozi hao, Rais Magufuli amewapongeza kwa kuteuliwa kuziwakilisha nchi zao hapa nchini na ameahidi kuwa Tanzania itaendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati yake na nchi hizo.

Rais Magufuli ametoa wito kwa Mabalozi hao kutilia mkazo ushirikiano katika masuala ya kiuchumi yakiwemo kuwahamasisha wafanyabiashara na wawekezaji wa nchi hizo kuja kufanya biashara na kuwekeza hapa nchini, hususani katika viwanda, kilimo, utalii na utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii na kwamba Serikali itakuwa tayari wakati wote kujenga mazingira bora ya kufanikisha biashara na uwekezaji huo.

Aidha, Rais Magufuli amewaomba Mabalozi hao kufikisha salamu zake kwa viongozi wa nchi zao, na kuwakaribisha kuitembelea Tanzania ili kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment