Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Thursday 21 December 2017

NAIBU SPIKA TULIA ATIMIZA AHADI YAKE KWA WANA BUJELA

 Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dk. Tulia Ackson akikabidhi vifaa vya ujenzi kwaajili ya shule ya Sekondari ya Bujela iliyopo Wilayani Rungwe mkoani Mbeya ikiwa ni utekelezaji wa ahadi zake alizozitoa. 
 Wanafunzi wa Bujela  na walimu wao wakiwa katika picha na Naibu Spika.
 Naibu Spika Dk. Tulia Ackson akikabidhi mabati kwaajili ya ujenzi wa Kanisa.
 Dk Tulia akiwashukuru waumini wa Kanisa baada ya kukabidhi msaada wa Mabati.
Naibu Spika Dr Tulia Ackson amefanya ziara katika baadhi ya maeneo Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya ikiwa ni kutekeleza baadhi ya ahadi alizowahi kuzitoa katika kusaidia maendeleo, kwanza alianza kwa kutoa vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni tano katika shule ya sekondari Bujela

Akiwa katika shule ya Bujela Dr Tulia alisema “Ndugu zangu niwasihi jambo moja ambalo hata Rais Magufuli husisitiza, tusiingize siasa kwenye mambo ya maendeleo kwasababu  bila hivyo hatutapiga hatua, leo kama TULIA TRUST tuliahidi vifaa vyenye thamani ya Milioni tano na tayari tumetekeleza kwa kuja navyo vikiwemo bati, mbao, mchanga, saruji, chokaa, rangi, vioo, nondo."

“Tunafanya haya yote kwa ajili ya kuhakikisha tunawatengenezea watoto wetu mazingira mazuri ya kujisomea na baadae watuletee maendeleo sisi wazazi wao hivyo niwaombe viongozi wote tushikamane”  alisema Dr Tulia

Safari ikaendelea hadi katika Kanisa la Bujela ambalo liliharibiwa kwa upepo uliosababishwa na mvua huko pia  Dr Tulia alichangia jumla ya mabati 100 Kwa ajili ya kukamilisha ukarabati wa kanisa hilo ambalo tayari ujenzi wake ulianza kwa jitihada za waumini wenyewe kuchangishana kiasi cha fedha.

Dr Tulia aliwahimiza waumini pamoja na viongozi wa dini kuendelea kuliombea taifa la Tanzania amani pamoja na kumuombea Rais Magufuli ili aendelee kuiongoza nchi salama.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment