Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Sunday 30 July 2017

WIZARA YA AFYA YATOLEA UFAFANUZI KUHUSU MAFUNZO YA UTARAJALI

KUMEKUWEPO na upotoshaji wa mafunzo ya utarajali (Internaship programme) bila malipo yaani fedha za kujikimu wakati wa mafunzo hayo kwa baadhi ya wanaotarajia kuanza mafunzo kwa vitendo mapema mwaka huu.

Taarifa kwa umma, iliyotolewa na Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto kupitia kwa Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikali-Afya, Nsachris Mwamwaja inasema kwa sasa hakuna ‘intern’ aliyepangiwa kuanza mafunzo hayo kwani tunasubiri watoke waliopo kwenye mafunzo.

"Barua iliyodukuliwa na kusambaa kwa lengo la kupotosha wataraji hao ilikuwa ni kwa ajili ya wataraji (intern) kutoka nje ya nchi ambao kwa sheria hawalipiwi na Serikali ya Tanzania," ilisema taarifa hiyo ya Mwamwaja.

Aidha wapo ‘intern’ wawili ambao wanasoma nchini China na mwingine Algeria masomo yao yalihitaji mafunzo kwa vitendo kabla ya kumaliza na kwa kuwa ilikua lazima warudi vyuoni mwezi Oktoba waliomba kufanya mafunzo hayo  kwa kujigharimia  pamoja na kuwa ni watanzania na wazazi wao walikuwa wameridhia hilo kwa maandishi ili warudi  mapema kumalizia program yao ya udaktari.

Hivyo ni watanzania wawili tu wameshapata barua yenye kuwataka  kujilipia kwa mazingira hayo hakuna wengine waliyepewa barua ya kuruhusiwa kwenda mafunzo ya utarajali (internship) bila malipo.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment