Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 25 July 2017

TAASISI YA WOMEN TEARS YASAIDIA WAZEE MOSHI VIJIJINI



 Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya Kiserikali ya Women Tears Ltd, Doreen Kimbi akikabidhi misaada ya mablankenti kwa wazee mbalimbali wa Moshi Vijijini hivi karibuni ikiwa ni saada wa asasi hiyo kwa wazee hao wa;lio na mahitaji mbalimbali. Zaidi ya wazee 200 walinufaika na misaada hiyo.
Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya Kiserikali ya Women Tears Ltd, Doreen Kimbi akikabidhi misaada ya mablankenti kwa wazee mbalimbali wa Moshi Vijijini hivi karibuni ikiwa ni saada wa asasi hiyo kwa wazee hao wa;lio na mahitaji mbalimbali. Zaidi ya wazee 200 walinufaika na misaada hiyo.
ZAIDI ya wazee 214 wa Moshi Vijijini ambao wanaotegemea msaada  wa matibabu na mahitaji mengine muhimu ya kibinadamu kutoka kwa wasamaria wema kwa ajili ya kujikimu kimaisha, wamepatiwa msaada wa jora tatu za nguo za baridi, baada ya kufadhiliwa na asasi isiyo la kiserekali la Women Tears Limited.

Mkurugenzi wa Shirika hilo, Doreen Kimbi alisema pamoja na mambo mengine kundi jingine la wazee watakaotambuliwa na asasi yake wataanza kunufaika na uchunguzi wa afya utakaofanywa na jopo la madaktari kutoka Hospitali ya Rufaa ya KCMC.

“Kuna mabadiliko makubwa ya hali ya hewa kwenye mkoa wetu, hasa ongezeko la baridi katika Wilaya ya Moshi na miji ya jirani, wanaopata tabu, wengi wao ni wazee hawa ambao wanategemea misaada ya kibinadamu. Kama Shirika ambalo linashughulika na kundi hili, tumeamua kutoa majora matatu yenye masweta kwa wazee zaidi ya 214 ili wajisitiri,”alisema Doreen

Alisema licha ya shirika hilo kutokuwa na wafadhili kwa sasa lakini amelazimika kutoa fedha zake mfukoni ili kuwasaidia wazee hao kutoka vijiji vya Kitandu Mkwaleni, Kitandu Minja na Kitandu Shinga vilivyopo Kata ya Uru Kusini.

Kuhusu uchunguzi wa afya, Mkurugenzi huyo alisema bado anahaha kutafuta fedha kwa wafadhili mbalimbali kwa ajili ya kuendesha zoezi maalumu la uchuguzi huo bila malipo, kwa kuwa idadi kubwa ya wazee wasiojiweza wanasumbuliwa na saratani ya tezi dume, kisukari na magonjwa ya moyo.

Shirika hilo limesisitiza pia kwamba liko tayari kuwawezesha wazee hao kufikia gharama za matibabu kwa kuwakatia vitambulisho vya Bima ya Afya ya Jamii  (CHF).

Mbali ya kusaidia wazee, pia shirika hilo linapigana kutoa elimu kwa raia kuachana na ukatili na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini (Albinism).

Wakati wazee wasiojiweza wakihitaji misaada kadha wa kadha, bado taifa lina deni kubwa la changamoto ya kukwama kwa miaka 14, sera ya taifa ya wazee ya mwaka 1999 ambayo haijapelekwa Bungeni kutungwa na kuwa Sheria.

Mkwamo ambao unatajwa kama udhaifu unaochangia kushamiri kwa matukio ya ukatili na kutojumuishwa kwa wazee hao katika ajenda ya maendeleo.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment