Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 4 July 2017

RAIS MAGUFULI KUZINDUA MRADI WA UBORESHAJI HUDUMA ZA MAJI NA MAZINGIRA SENGEREMA LEO



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akinunua Karanga kutoka kwa Mmachinga anayefanya biashara katikati ya jiji la Mwanza.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa katikati ya jiji la Mwanza waliokusanyika kumpokea.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wakazi wa katikati ya jiji la Mwanza wakati akielekea Uwanja wa Nyamagana kuangalia mechi kati ya Buhongwa United na Timu ya Nyamwaga.
RAIS Dkt. John Magufuli, yupo mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

Rais Magufuli aliwasili jana Julai 3 mwaka huu jijini Mwanzan  na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Mwanza.

Akiwa mkoani humo, Rais Magufuli atakuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mradi wa  uboreshaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Sengerema utakaofanyika leo Julai 4, 2017.

Katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza, Rais Dkt. Magufuli aalikutana na kamati ya amani ya viongozi wa dini na  kuwashukuru viongozi hao kwa sala na dua zao na amewataka waendelee kuwahimiza waumini wao kuliombea Taifa ili liepukane na vitendo vya rushwa ambavyo ni adui wa maendeleo.

Akiwa njiani kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza katika eneo la Bwiru kuelekea Ikulu ndogo ya Mwanza, Rais Magufuli msafara wake umesimamishwa mara kwa mara na wananchi waliojaa barabarani na kuamua kuzungumza nao ambapo amewahakikishia kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imepania kupambana na ufisadi kwa lengo la kuwaletea maendeleo Watanzania bila kujali tofauti za dini au Siasa.

Aidha, amewahakikishia wananchi hao kuwa Serikali yake imedhamiria kuondoa kero mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufuta baadhi ya kodi zenye kero na kuwapatia vitambulisho wafanyabishara wadogo wadogo, maarufu kama Wamachinga, ili waweze kufanya biashara zao bila kusumbuliwa.

Akiwa eneo la Nyamagana jijini Mwanza, Rais alitembea kwa miguu huku kuwasalimu wananchi waliokuwa wakimshangilia na kuzuia msafara wake. Rais Magufuli pia alikwenda  Uwanja wa Mpira wa Nyamagana na kuungana na baadhi ya wananchi waliokuwa wakiangalia mechi ya mpira wa miguu  kati ya timu ya Buhongwe na Nyamwaga.

Rais Dkt. Magufuli pia amefurahishwa na maendeleo ya ujenzi wa barabara ya kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza hadi katikakati ya jiji ambao gharama za ujenzi wake zilitokana na fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya sherehe za Muungano.  


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment