Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Sunday 2 July 2017

NUKUU ZA RAIS JOHN MAGUFULI HII LEO KATIKA UPANUZI WA BANDARI YA DAR ES SALAAM



NUKUU MBALIMBALI ZA RAIS DK JOHN MAGUFULI WAKATI WA AZKIZUNGUMZA HII LEO KATIKA UZINDUZI WA UPANUZI WA BANDARI YA DAR ES SALAAM.
****************
#"Inaonekana kina mama wanaosimamia mashirika ya maendeleo wanafanya kazi nzuri, hata huu mradi ambao umegharimu zaidi ya bilion 900 umewezeshwa na wao," Rais John Magufuli 
           
#"Ufanisi na utendaji mzuri wa reli ya standard gauge utategemea ufanisi wa bandari hii, hivyo mtaona ni jinsi gani ni muhinu. Upanuzi huu utaongeza shehena ya mizigo na hivyo kuwezesha serikali kukusanya mapato,"  Rais John Magufuli                        

#"Unatarajiwa kukamilika kwa miezi 36 kama mkataba unavyosema, lakini,nataka miezi 30 iwe imekamilika lakini ikiwezekana hata miezi 28, fedha zipo sasa wakae miezi 36 hapa wanafanya nini," Rais John Magufuli                        

#"Ilitakiwa hii bandari iltakiwa iwe imepanuliwa zamani, wafanyabiashara walikuwa wanalamimika bila kusema sababu, tulikuwa na eneo ambalo halitoshi labda ulete mitumbwi na viboti hivi. Tulikuwa tunasema tuna bandari lakini kumbe upande mmoja ni bandari na upande mwingine ni mwalo," Rais John Magufuli                        

#"Ikishakamilika bandari hii itakuwa ni ya mfano kwa sababu zitakuwa meli nyingi zinakuja kwa wakati mmoja, kutakuwa hakuna ucheleweshaji labda kama TPA wacheleweshe kwa makusudi na hao watakaochelewesha ndio tutalala nao vizuri," Rais John Magufuli                        

#"Pakiwa na facility nzuri hapa tutakuwa tunapromote uchumi wa nchi zingine. Bahati nzuri sisi ni wanachama wa SADC na EAC... hivyo watu kama milioni 500 watanufaika na bandari hii," Rais John Magufuli. 
                      
#"Serikali ya wamu ya tano imedhamiria kuboresha miundombinu ya usafiri na kudhihirisha hilo, tunaendelea na upanuzi wa bandari mbalimbali, viwanja vya ndege na barabara," Rais John Magufuli    
                   
#"Bandari mmeanza vizuri lakini nataka kwenye hizi ICDs, hizi ziliwekwa kwa ajili mizigo ikijaa hapa ndio ipelekwe kule lakini sasa hivi inapelekwa hata kabla haijajaa na kuna kamchezo fulani...mizigo inasemwa ni transit lakini inauzwa humu humu, kuna kampuni fulani inafanya huo mchezo wa kukwepa kodi fuatilieni hilo," Rais John Magufuli         
               
#" Kuna vichwa 13 vya treni vimeshushwa hapa lakini havijulikani ni vya nani, tena inasemekana ni vibovu na TRL wamesema hawajaagiza na wala hwajasaini mkataba wowote. Hamkuuliza vya nani baada ya meli kuondoka ndio mnauliza, siku nyjngine si watakuja kushusha hata na vifaru au makontena ya sumu," Rais John Magufuli                       

#"Sijui haya mavichwa mtafayanyia nini, lakini hili nj lazima lisemwe ili Watanzania wafahamu. Tutangulize uzalendo wa nchi yetu      
                 
#"Niwaombe wanasiasa wanaoshindwa kucontroll midomo ya, wanaosema kuwa hawa watu wameshikwa kwa muda mrefu, tunashindwa kujua hata kuna watu kule Marekani walikaa Guantanamo muda nrefu, katika hali hiyk kwanini usifanye watu wafikiri na wewe ni mmoja wao. Msitufanye tukafika huko," Rais John Magufuli.             
          
#"Kwanini hata siku moja mtu asijitokeze kuulani watu wanaouawa bila hatia kule. Lakini kwa kuta sifa za kisiasa, mtu anatoka anasema hawa watu wako ndani muda mrefu, kuna ndugu zetu wanakufa kule...nataka polisi mfanye kazi yenu, hawa wanaoropoka waisaidie polisi, msiogope sura, awe na mwendo wa haraka, polepole au kukimbia, mkamateni ili kusudi aisaidie polisi akiwa kule ndani," Rais John Magufuli                
       
#"Juzi mtu amekamatwa na uniform 5000 za jeshi na inaonekana anahusika na hao walioko ndani, halafu unasema wamekaa muda mrefu, au na wewe ni miongoni mwa waliogiza hizo uniform za jeshi," Rais John Magufuli.    
                   
#"Endeleeni kujenga heshima ya bandari, rushwa iwe ni marufuku, halafu muda pia... mtu akifika hapa akae muda mfupi na aondoke, hata kama anasafirisha pini ifike inapokwenda na sio ipotelee njiani," Rais John Magufuli


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment