Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 23 June 2017

POLISI YATOA TAHADHARI KWA WAHALIFU SIKU YA EID EL FITRI



JESHI la Polisi nchini limetoa tahadhari kwa watu au vikundi vya watu vilivyopanga kufanya uhalifu klatika siku ya siku kuu ya Eid El Fitri.

Taariofa iliyotolewa na Jeshi hilo kupitia kwa Msemaji wake Advera Bulimba imewataka  wananchi kuwa makini katika suala zima la ulinzi na usalama wa maisha na mali zao.   

"Kipindi kama hiki cha sikukuu baadhi ya watu hupenda kutumia fursa hiyo kufanya vitendo vya uhalifu na vitendo vingine ambavyo huhatarisha usalama wa watu na mali zao,"ilisema taarifa hiyo.

Naibu kamishna huyo wa Polisi, Advera Bulimba alisema Jeshi la Polisi nchini,  limejipanga kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama katika mikoa yote kuhakikisha kwamba  wananchi wanasherehekea Sikukuu katika hali ya amani  na utulivu.  

Aidha, ulinzi umeimarishwa kwenye maeneo yote, yakiwemo maeneo ya kuabudia, fukwe za bahari, sehemu za starehe na maeneo mengine ambayo yatakuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu. 

"Vilevile,  Jeshi la Polisi linawatahadharisha watumiaji wa vyombo vya moto barabarani kuwa makini  na kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani,  Jeshi la Polisi halitasita kuwachukulia hatua kwa wale wote watakaovunja  sheria na kanuni za usalama barabarani kwa mabereva kutumia vilevi, bodaboda kubeba  mishikaki, kwenda mwendo kasi pamoja na kupiga honi hovyo," taarifa hiyo ilieleza.

Pia, tunawataka  wananchi wote kuwa wepesi katika  kutoa taarifa kwa kupitia  namba za simu za bure 111 au 112  pindi wanapoona viashiria vyovyote vya uhalifu katika maeneo yao ya makazi ama maeneo ya biashara.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment