Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 30 May 2017

TAASISI YATAKA WANAFUNZI KUSHIRIKI MASHINDANO YAKUONGEZA UFIKIRI

Badhi ya majaji katika mashindano ya chemsha bongo kwa wanafunzi wa shule za sekondari za mkoa wa Dar es Salaam yaliyoandaliwa na Taasisi ya An-Nahl , kutoka kushoto ni Mtoka Fikirini, Katibu wa vijana wa taasisi hiyo, Abdulkarim Kichechele na Meneja Matukio, Baruani Fikirini.

Viongozi wa Taasisi ya An-Nahl wakifuatilia maswali ya wanafunzi katika mashindano ya chemsha bongo kwa wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mbaraka Maseneke, Amir wa Vijana Anthony Mahimbila, Mratibu wa Habari, Farid Mbaraka na Mweka Hazina wa taasisi hiyo, Andallah ndelele, mashindano hayo yamefanyika katika msikiti wa Kichangani, uliopo Magomeni.

Baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari za jijini Dar es Salaam, wakifuatilia maswali yanayoulizwa katika mashindano hayo ya chemsha bongo.

TAASISI ya An-Nahl imezindua mashindano ya chemsha bongo kwa wanafunzi wa shule za sekondari, huku ikwashauri wanafunzi wengi kushiriki mashindano mbalimbali yenye lengo la kuwasaidia katika kuongeza ufikiri na kupanua wigo wa mawazo.

Ushauri huo umetolewa na Amir wa Vijana wa taasisi hiyo, Anthony Mahimbali wakati akifungua mashindano hayo ambapo ameeleza kuwa, lengo la kuanzisha mashindano hayo ni kuhakikisha wanafunzi wanakuwa na uwezo mkubwa wa kufikiri na kutatua changamoto zao wenyewe.

Amesema, masindano hayo kwa sasa mashindano hayo yanashirikisha shule za jiji la Dar es Salaam pekee lakini wanajipanga kuhakikisha wanawafikia vijana wote nchini.

“Mashindano haya hufanyika kila mwaka katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, safari hii tumealika shule karibu 200 ambazo ni za serikali na binafsi, kwasababu mashindano haya si tu kwa ajili ya kujifunza dini lakini kuongeza uelewa kwa sababu yanaulizwa maswali tofauti,” alisema Mahimbali.

Mahimbali amesema, katika mashindano hayo wanafunzi huulizwa maswali ya papo hapo yanayohusu dini, masomo ya darasani na mazingira ya jamii kwa ujumla ili kutoa fursa kwa vijana hao kuchanganua mambo mbalimbali na kuongeza wigo wa kufikiri.

Amefafanua kutokana na mashindano hayo kuhusisha maswali ya darasani yamewasaidia wanafunzi wengi kusoma na kukumbuka kuhusu masomo yao, hatua ambayo imewasaidia katika kuongeza ufaulu katika masomo yao.

Mchujo wa mashindano hayo katika ngazi ya wilaya unatarajiwa kufanyika Jumapili ijayo ambapo umegawanywa katika wilaya tatu ambazo ni Kinondoni, Ilala na Temeke ili kupata shule 15 zitakazoungana na bingwa mtetezi katika fainao itakayofanyika Juni 17 katika ukumbi wa city garden, Gerezani.

Mchujo huo ambao katika wilaya ya Ilala utafanyika katika shule ya Seminari ya Ilala Islami, Kinondoni shule ya sekondari Ridwaa na Temeke katika Chuo Kikuu cha Elimu Dar es Salaam (DUCE).


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment