Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Friday 5 May 2017

MWENGE WA UHURU WAKIMBIZWA MADABA

 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari St Getruda iliyopo Halmashauri ya Madaba, Wilaya ya Songea, Mkoani Ruvuma wakiulaki mwenge wa uhuru jana,uliofika shuleni hapo kwa ajili ya kutoa ujumbe wa mwenge kwa mwaka 2017 ambapo kiongozi wa mwenge  kitaifa Amouru Hamad Amour amewataka wanafunzi hao kuhakikisha wanaongeza bidii katika masomo yao ili waweze kufanikisha ndoto walizonazo  kimaisha. Picha zote na Muhidin Amri.
 Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dkt Binilith Mahenge kushoto,akipokea mwenge wa uhuru jana kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka katika kijiji cha Mahanje halmashauri ya wilaya ya Madaba mara baada ya mwenge huo kumaliza mbio zake mkoani Njombe
 Kiongozi wa mbio za mwenge wa  uhuru kwa mwaka 2017, Amour Hamad Amour,akimsikiliza mwenyekiti wa Mahanje Saccos Wilayani Songea, Arika Mgina mara baada ya  kuangalia shughuli mbalimbali zinazofanyika katika Saccos hiyo na kupongeza uongozi kwa kazi nzuri inayofanya ya kuwainua  wananchi kiuchumi. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Shafi Mpenda, akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema.
 Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2017 Amour Hamad Amour akiinua ndoo ya maji jana mara baada ya kuzindua mradi mkubwa wa maji safi na salama katika kijiji cha Lilondo halmashauri ya wilaya ya Madaba,wakati wa siku ya kwanza ya mbio za mwenge wa uhuru mkoani Ruvuma,kulia ni mkazi wa kijiji hicho Ostella Mwenda.
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2017 Amour Hamad Amour (kulia) na Mkimbiza mwenge kitaifa Frederick Ndahani wakiomba dua ya kuwaombea waasisi wa mwenge wa uhuru Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa kwanza wa Zanzibar hayati Abeid Karume katika kijiji cha Lutukira katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba,mara baada ya kukagua kikundi cha vijana waendesha boda boda wanaojishuhulisha na kilimo cha mahindi kijijini hapo.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment