JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam wamemwachia huru Msaanii wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki maarufu Ney wa Mitego.
Polisi wamemwachia huru msanii huyo jioni ya leo ikiwa ni muda mfupi baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk Harison Mwakyembe kuliagiza jeshi hilo kumwachia huru msaani huyo huku akiiomba Baraza la Sanaa la Taifa lililokuwa limeagiza kushikiliwa kwake na kuzuia upigwaji wa Mziki wake mpya wa 'WAPO' pia iuruhusu wimbo huo kupigwa katika vituo vya redio na maeneo mengine.
Msanii Ney alikuwa akishikiliwa na Jeshi la
Polisi baada ya kumkamata juzi mkoani Morogoro na kumsafirisha hadi jijini Dar
es Salaam kufuatia amri ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kile
kilichodaiwa ni wimbo huo kukosa maudhui na kukiuka sharia za Basata.
Waziri Mwakyembe alifuatilia sakata hilo la
kukamatwa Ney na baadae Basata kufahamisha sababu za kumkamata na kutakiwa
kuhojiwa juu ya nyimbo yake ya ‘Wapo’ lakini pia Rais alimuagiza kufuatilia
suala hilo na kuona namna ya kulimaliza kwakuwa haoni kosa katika wimbo huo.
Aidha Mwakweye amesema Rais Magufuli aliomba Ney
achiwe hivyo nayeye akiliagiza Jeshi la Polisi kumuachia huru msanii huyo.
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment