Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Sunday 5 February 2017

WASANII, WATU WENYE MAJINA MAKUBWA NDIO WANAONEKANA ZAIDI KATIKA ATHARI ZA MADAWA YA KULEVYA

Na Lilian Lundo – MAELEZO  Dodoma
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Nape Nnauye (pichani) amesema kuwa wasanii na watu wenye majina makubwa ndio wanaoonekana zaidi katika athari za madawa ya kulevya ingawa wapo wengi katika jamii wanayotumia dawa hizo.

Nape ameyasema hayo  Mjini Dodoma alipokuwa akitoa majibu kwa waandishi wa habari waliotaka kujua namna ambavyo wizara yake imelipokea sakata la kukamatwa kwa wasanii ambao wanatuhumiwa kutumia madawa ya kulevya.

“Kama wizara inayosughulikia suala la wasanii tunaunga mkono juhudi zozote za kupambana na jambo hili kwa sababu mwisho wa siku sehemu ya wadau wetu wanaathirika, hivyo basi juhudi za kupambana nalo zinaokoa wadau wetu,” alifafanua Nape Nnauye.

Aliendelea kwa kusema kuwa kama wizara inayosimamia wasanii wamekuwa wakijadili na kuzungumza juu ya athari hizo za madawa ya kulevya kwa wasanii, aidha wapo wasanii ambao Serikali imewasaidiwa kupata matibabu kutokana na athari za madawa hayo, akiwemo mwanamuziki Rehema Chalamila anayefahamika kama Ray C.

Aidha amesema kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa huo hivyo hawajibiki kuuliza Wizara hiyo anapotaka kuchukua hatua zozote kwa wasanii waliopo ndani ya mkoa anaosimamia, lakini anapohitaji anaweza kuiuliza wizara hiyo.

Nape amesema kuwa ni kazi kubwa sana kwa mtu kutengeneza jina (brand)  lakini ni rahisi sana kubomoa, hivyo basi ni vyema busara ikatumika katika kuwashughulikia waathirika, vile vile watu wasihukumiwe kwa tuhuma.

Hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitangaza majina ya watu wanaotuhumiwa kuuza ama kutumia madawa ya kulevya wakiwemo wasanii, maaskari na wafanyabiashara na kuwataka kuripoti Polisi kwa ajili ya mahojiano.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment