Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 17 January 2017

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA KINGDOM LEADERSHIP NETWORKS

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwenyekiti wa Taasisi ya Kingdom Leadership Network Tanzania Ibrahimu Kaduma aliyemtembelea Makamu wa Rais na kumuelezea mikakati ya kuanzisha Chuo cha Joseph Business School.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akizungumza na Mwenyekiti wa Taasisi ya Kingdom Leadership Network Tanzania Ibrahimu Kaduma aliyemtembelea Makamu wa Rais na kumuelezea mikakati ya kuanzisha Chuo cha Joseph Business School kushoto ni Meneja Mradi Dkt Charles Sokile.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiwa kwenye picha ya pamoja na ujumbe wa Taasisi ya Kingdom Leadership Network Tanzania uliomtembelea ofisini kwake, Ikulu jijini Dar es Salaam.
************
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameuhimiza uongozi wa Taasisi ya Kingdom Leadership Network Tanzania(KLNT) kuharakisha mchakato wa kuanzisha kituo cha Joseph Business Centre(JBC) kwa ajili ya maboresho ya uchumi wa nchi na ukuzaji viwanda.  

Moja kati ya malengo ya chuo hicho ni kusaidia na kuhimiza maendeleo ya viwanda na kupitia ugundunzi ya mawazo ya biashara na viwandani (Incubation Centre) ya Sayansi, Teknolojia, Kilimo cha biashara, uzalishaji na utalii.

Makamu wa Rais ametoa kauli ofisini kwake Ikulu Jijini Dar es Salaam leo alipokutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa  Taasisi ya Kingdom Leadership Network Tanzania(KLNT) ambao walimtembelea Makamu wa Rais kumweleza hatua ambazo wamefikia katika uanzishaji wa kituo na Chuo hicho.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema wazo la uanzishaji wa Kituo na Chuo hicho ulitolewa na Dkt Bill Winston ambaye ni Mwanzilishi wa Chuo cha Joseph Business School, Chicago nchini Marekani na Bill Winston Ministries mwaka jana katika Maombezi ya Taifa( National Prayer Breakfast) ambaye yeye alikuwa mgeni rasmi katika maombi hayo, anasema aliupokea kwa furaha mpango huo kwa sababu kituo na chuo hicho kitasaidia watanzania wengi kupata elimu na ujuzi wa kuimarisha biashara zao wakati taifa likielekea kwenye uchumi wa Viwanda.

Amesema hatua za uanzishwaji wa kituo na Chuo hicho hapa nchini ni fursa pekee na nzuri kwa Watanzania kujifunza ubunifu na ugunduzi katika biashara, maadili ya uongozi katika biashara ili kuongeza ufanisi katika biashara zao kwa ajili ya manufaa yao na taifa kwa ujumla hasa katika ulipaji wa kodi.

Kwa Upande wake, Mwenyekiti wa bodi Taasisi ya Kingdom Leadership Network Tanzania Ibrahimu Kaduma, Mkurugenzi wa Mradi wa JBC Dkt Charles Sokile wamemhakikishia Makamu wa Rais kuwa hatua ambazo wamefikia kwa sasa katika uanzishaji wa kituo na Chuo hicho ni nzuri ambapo mpaka sasa wamepata majengo kwa ajili ya ofisi na maeneo ya kufundishia na hatua za usajili wa chuo hicho zipo katika hatua za mwisho.

Watendaji wa KLNT wamesisitiza kuwa wanataka kushirikiana ipasavyo na Serikali katika uanzishaji wa kituo na chuo hicho ambacho kitatoa elimu ya biashara hasa ugunduzi wa mawazo ya biashara nchini kama hatua ya kutekeleza kwa vitendo dhana ya kuelekea kwenye uchumi wa viwanda nchini.

Taasisi ya  KNLT ni taasisi ya kizalendo, ambayo inashugulikia maswala ya uadilifu kwenye uongozi, uchumi, uwekezaji na katika biashara imekuwa ikifanya shughuli zake hapa nchini kwa faida na tija ya maendeleo ya taifa.  

Katika kituo hicho cha JBC kutakuwa kitengo cha kusaidia fedha za mitaji kwa wahitimu waliofanikiwa kulelewa mawazo ya kibiashara yenye tija kwa Taifa, na  mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Marekani.


Kulingana na maelezo ya watendaji hao tawi la Chuo cha Joseph Business School (JBS) hapa nchini chini ya chuo cha Kingdom Leadership Institute(KLI)  ambacho kitatoa mafunzo mbalimbali ya biashara, maadili ya uongozi na ugunduzi wa mawazo ya biashara ili kusaidia mamia ya Watanzania kuimarisha shughuli zao za kiuchumi. 


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment