Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Tuesday 10 October 2017

MKUU WA WILAYA YA TARIME AFUNGUA KONGAMANO LA WATOTO KUELEKEA SIKU YA KIMATAIFA YA MTOTO WA KIKE OKTOBA 11, 2017

 Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Grolius Luoga akizungumza na watoto wakati wa kongamano la kuzuia mimba za utotoni kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike yatakayofanyika tarehe 11 Oktoba  2017 katika wilaya ya Tarime mkoani Mara.
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto,Magreth Mussai akiwasalimia watoto waliojumuika kwenye kongamano la kuwajengea watoto uelewa wa kujilinda dhidi ya ndoa za utotoni siku moja kabla ya maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Kitaifa yatakayofanyika tarehe 11 Oktoba, 2017 wilaya ya Tarime mkoani Mara.
 Mwakilishi wa watoto wilayani Tarime Anna Simon akiwakilisha watoto wa wilaya ya Tarime kutoa salamu za watoto kwa, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Bw. Glorius Luoga(hayupo pichani) wakati wa mjadala wa ulinzi wa watoto katika ngazi ya familia, shuleni, mtaani na jamii  kwa ujumla.
 Baadhi ya watoto, wazazi, walezi na wazee wa mila katika wilaya ya Tarime wakifuatilia kwa makini nasaha za Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Grolius Luoga(hayupo pichani) kuhusu wajibu wa kuwalinda watoto dhidi ya mimba za utotoni katika wilaya ya Tarime, mkoani Mara.
  Mkuu wa Wilaya ya Tarime,Grolius Luoga akipokea zawadi ya vitabu kutoka kwa mwakilishi wa watoto Anna Simon mara baada ya kufungua kongamano la watoto wilaya ya Tarime, mkaoni Mara.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Grolius Luoga akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa ulinzi na usalama wa mtoto katika ngazi ya jamii wilaya ya Tarime, mkoani Maramara baada ya kufungua kongamano la watoto.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment