Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Wednesday 5 July 2017

TTCL YAJA NA HUDUMA MPYA YA TTCL PESA KWA WATEJA WAKE

Kampuni ya Simu ya Tanzania (TTCL) imewataka Watanzania kuwa wazalendo na kutumia huduma za mtandao huo ikiwemo huduma ya TTCL Pesa iliyoanzishwa mwaka huu.

Mtunza fedha Fedha wa Idara ya TTCL Pesa, Liliane Hosea (pichani) ametoa kauli hiyo katika maonesha ya 41 ya biashara ya kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere, barabara ya Kilwa.

"Kupitia TTCL Pesa wanaweza kupata huduma mbalimbali za kutuma na kupokea pesa, pamoja na huduma nyingine za miamala ya kifedha ambayo mtu anaweza kutumia katika kupata huduma," amesema Liliane.

Aidha, amesema mbali na huduma hiyo lakini pia wateja watakaotembelea banda lao wanaweza kupata huduma zingine mbalimbali ikiwa ni pamoja na simu za kisasa, vifaa vya intaneti pamoja na intaneti ya kasi ya 4G.

Naye, Rashid Majid ambaye ni Ofisa Bidhaa wa TTCL amesema, katika maonesho hayo wana simu za mezani za kisasa pamoja na vifaa vingine ikiwemo kamera za usalama.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment