Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Wednesday 5 July 2017

TFF YASEMA UCHAGUZI MKUU UPO PALEPALE AGOSTI 12 MJINI DODOMA

 
Sikiliza video hii

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewataka wanafamilia wa mchezo wa soka nchini kuwa na subira, kwakuwa Kamati ya uchaguzi mkuu wa shirikisho imeundwa upya na kilichobaki ni Mwenyekiti wake, Revocatus Kuuli kuwaita wajumbe wa kamati hiyo.


Msemaji wa shirikisho hilo, Alfred Lucas amesema, tayari kamati hiyo imeshafanyiwa marekebisho kwa kuondoa baadhi ya wajumbe na kuweka wajumbe wengine wapya.


"Mambo yote yako tayari, wanafamilia wa soka wawe na subira tu, kwasababu wajumbe wameshateuliwa na kilichobaki ni Mwenyekiti kuwaita, kwahiyo nafikiri ndani ya siku mbili hizi tutawatangazia mashabiki wa mpira rasmi," amesema Luca.


Lucas pia amesisitiza kuwa tarehe ya uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo bado haijabadilika bali unatarajiwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu mjini Dodoma.


Aidha, amesema kilichosababisha kamati ya kwanza kuvunjwa ni baada ya Kamati ya Utendaji ya TFF kujidhihirisha kuwepo kwa kutokuheshimiana na uelewa mdogo, mgongano wa maslahi pamoja na nidhamu.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment