Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.

Have you got a good story?

Share your story, discuss the issues with Dailynews Blog.





Nafasi Ya Matangazo

Wednesday 5 July 2017

NHIF WAFANYA USAJILI WA FASTA FASTA WA FAO LA TOTO AFYA KADI SABASABA

Shirika la Taifa la Bima ya Afya (NHIF) limeeleza azma yake ya kuwawezesha watoto wengi kuwa na bima ya afya, kupitia fao la Toto Afya Kadi inayotolewa katika maonesho ya Sabasaba. Anaandika Katuma Masamba.

Ofisa Masoko na Elimu kwa Umma wa NHIF, Hawa Duguza amesema, katika maonesho hayo watakuwa wakitoa vitambulisho vya bima siku moja baada ya mzazi kuwasilisha taarifa zote zinazohitajika.

"Tuko hapa kwa ajili ya kutoa elimu na kuhamasisha watu kujiunga na bima ya afya na hasa fao jipya la Toto Afya Kadi ambayo ni mahususi kwa watoto," amesema Hawa.

Amesema ili mzazi aweze kupata kadi ya Toto Afya Kadi kwa ajili ya mtoto wake atalazimika kuwasilisha vivuli vya kadi ya mtoto ya kuzaliwa na picha ndogo na baada siku moja atapewa kitambulisho cha mtoto wake.

Mbali na hilo amesema, kupitia maonesho hayo wanapokea malalamiko na changamoto mbalimbali kutoka kwa wateja wao na kuyafanyia kazi.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Post a Comment