Kamati
ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu kwa Wanawake (TWFA), imetangaza
majina ya wagombea 11 waliopitishwa kuwania nafasi mbalimbali katika
uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaofanyika Julai 8, mwaka huu mkoani
Morogoro.
Majina
ambayo yamepitishwa ni Amina Karuma, Rose Kisiwa, Somoe Ng’itu,
Theresia Mung’ong’o, Hilda Masanche, Salma Wajeso, Zena Chande,
Triphonia Temba, Mwamvita Kiyogoma, Jasmin Soudy na Chichi Mwidege.
Nafasi
zinazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu
Msaidizi, Mweka Hazina, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF na Wajumbe wanne
wa Kamati ya Utendaji.
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment